Skip to main content

SERIKALI KUWALIPA WANAOPISHA MIRADI YA MAENDELEO






Na Mwandishi wetu 

Serikali imesema imekua ikifanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha wananchi wanaopitiwa na miradi mbalimbali ya kimaendeleo wanalipwa stahiki zao katika maeneo yaliopitiwa na miradi ili kuhakikisha hakuna malalamiko kutoka kwa wananchi.

Akizungumza na wadau mbalimbali, Kamishana wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Nyanda Shuli, katika mdahalo ulioandaliwa na Taasisi ya HakiRasilimali ambapo amesema Tume hiyo imekua ikifanya kazi na wadau mbalimbali.

"Tume ya haki na utawala bora imekuwa ikifanya kazi na wadau mbalimbali ikiwemo kituo cha Sheria na haki za Binadamu(LHRC) na imekuwa ikipokea malalamiko ya aina tofauti tofauti kutoka kwa wananchi nakuyaripoti Mahakamani kupatiwa utatuzi"amesema Nyanda.

Aidha, katika mdahalo huo walijadili kwa kina namna sheria zinavyoweza  kumsadia mwananchi kupata haki zake pale mradi unapopita katika eneo lake ili aweze kulipwa fidia kulingana na hali halisi ya mali zilizopo

"Kuna baadhi ya mikanganyiko inayotokea wengine kutoridhika na fidia wanazolipwa hivyo kuamua kupeleka malalamiko mahakamani,hivyo inatakiwa elimu iendelee kutolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali"amesema Shuli

Kwa upande wake, Mwakilishi  kutoka Mradi wa  Bomba la Mafuta Gafi kutoka Unganda hadi Tanzania(ECOP) Fatma Msumi amebainisha kuwa  baadhi ya maeneo ambayo bomba hilo limepita Wananchi wamepatiwa stahiki zao kwa mujibu wa sheria za haki za Binadamu.

"Vingine ilitulazimu kukutana na wazee wa kimila kwanza kuzungumza nao kutokana na baadhi yao imanani zao na matambiko yao hufanyika kwenye makaburi au miti hivyo wengine kukataa kabisa kuhamisha makaburi yao na kuwalazimu wao kuangalia namna ya kukwepa maeneo hayo ili kusitokee mkanganyiko' amesema

Nakuongeza kuwa "Kiukweli  Mradi huu wa bomba la mafuta Ghafi la Afrika Mashariki kila maeneo ramani yake imeonyesha litapita kuna ofisi ambayo watumishi wake wamekuwa wakizungumza na viongozi wa kijiji, kitongoji ,kimila kuweka mazungumzo ya pamoja kuhusu raslimali zao kama kuna uwezekano wa kulipwa fidia wapishe maradi "

Kwa upande wake,Mtaalamu wa masuala ya haki za binadamu kutoka kituo cha Sheria na haki za binadamu LHRC, Joyse Komanya amesema kituo hiko kimekuwa kikipokea malalamiko ya ukiukwaji wa haki za binadamu haki raslimali kwa wanaopisha miradi kwani wengine hulipwa fidia ndogo ikilinganishwa na mali walizonazo hivyo nao wamekuwa wakiwasaidia kwa kuwapatia Elimu namna ya kupata haki zao

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...