Skip to main content

TUGHE YATOA RAI KWA WAAJIRI KUWAPA WAFANYAKAZI HAKI YA KUJIUNGA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI










Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) kimetoa rai kwa Waajiri nchini kuwapa wafanyakazi wao haki ya kujiunga na Vyama vya Wafanyakazi ili kuleta tija katika maeneo ya kazi.

Akitoa salamu za TUGHE katika ufunguzi wa Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE iliyoanza jana Jumatatu Tarehe 26 Agosti 2024, Jijini Arusha, Katibu Mkuu wa TUGHE, Cde. Hery Mkunda amesema kuwa Vyama vya Wafanyakazi ni wadau muhimu sana katika kuchangia maendeleo ya Taasisi. 

Akizungumzia kuhusu Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE, Cde. Mkunda alieleza kuwa tangu mwaka 2018, TUGHE imekuwa na utaratibu wa kuandaa na kuratibu mafunzo ya pamoja yanayojumuisha washiriki toka Viongozi wa Matawi ya Chama na Mamlaka za Ajira au wawakilishi wao.

“Kwa niaba ya TUGHE niwashukuru sana Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE kwa kukubali kuwezesha na kushiriki mafunzo haya ambapo tayari matunda ya uwepo wa mafunzo haya ya kila mwaka yameanza kuonekana kwani Migogoro baina ya Watumishi na Waajiri imepungua sana na pale ilipojitokeza imekuwa ikipata utatuzi kwa njia ya majadiliano mahala pa kazi.”Cde. Mkunda

Mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti wa TUGHE Taifa, Ndg. Joel Kaminyoge, ambae pamoja na mambo mengine alisisitiza umuhimu wa kuhubiri wajibu na haki sehemu za kazi.

Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa ATE, Bi. Suzanne Ndomba-Doran akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo alisisitiza kuwa mada ya Haki za Msingi za Vyama vya Wafanyakazi ni elimu muhimu kwa Wanachama kwani wanapaswa kufahamu wajibu kwasababu hakuna haki bila wajibu na aliendelea kueleza kuwa Vyama Vya Wafanyakazi vina wajibu mkubwa wa kuleta utilivu,ufanisi na ukuaji wa tija sehemu za kazi na kuboresha mazingira na mahusiano mazuri baina ya Mwajiri na Mfanyakazi. 

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi Khadija Mwenda, ameipongeza TUGHE kwa kuandaa mafunzo hayo na kusisitiza kuwa amesisitiza kuwa kama nchi tunahitaji kuwa na nguvukazi yenye afya njema ili kuleta tija katika maeneo ya kazi hivyo nsuala la Afya na Usalama ni muhimu kuwa Agenda endelevu .

Mafunzo haya ya siku nne yamewakutanisha washiriki kutoka sehemu mbalimbali za kazi zikiwemo Wizara, Idara, Taasisi, Wakala wa Serikali, Mamlaka za Serikali, Bunge, Mahakama, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi za Afya za Serikali na zile za binafasi. Mafunzo hayo yatahitimishwa kwa Washiriki kufanya utalii wa ndani kwa kupata fursa ya kutembelea hifadhi ya  Taifa Ngorongoro.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...