Skip to main content

WASANII WA BONGO MOVIE KUPEWA TUZO ZA HESHIMA ZA KIMATAIFA

 



Na Mwandishi wetu

Wasanii wa Bongo movie wanatarajiwa kupewa heshima kimataifa kupitia Tuzo za Tamthilia zinazotarajiwa kuzinduliwa rasmi Agosti 24,2024 Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Meneja wa Kitengo cha Uhakiki kutoka Bodi ya Filamu nchini Boppe Kyungu amesema Serikali kupitia Bodi ya Filamu inazitambua tuzo hizo,ambapo pamoja na mambo mengine amewataka wadau wa Filamu nchini kuungana katika kuzifanikisha kwakuwa tuzo ni nyenzo ya kuboresha Sekta ya Filamu na Michezo ya Kuigiza nchini.

Aidha Kyungu ameongoza kuwa wadau wa Filamu wachangamkie Fursa hiyo kwani tuzo hizo zinaenda kuacha alama na kuona kasi mpya ya kutengeneza kazi zenye ushindani Kimataifa pamoja na kutangaza utalii na Utamaduni kupitia sekta ya Filamu nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mtendaji wa Tuzo za Tamthilia nchini Eliya Mjata amesema ujio wa tuzo hizo zinalenga kutoa fursa na wigo mpana kwa wasanii kuipa heshima tasnia na Nafasi kwa watayarishaji wa kazi za Sanaa ambao kwa sasa wanachukua nafasi kubwa kuchangia pato la taifa na kukuza Utamaduni na Kutangaza Utalii na Lugha ya Kiswahili.

Aidha ameongeza kuwa Kumekuwepo tuzo mbalimbali ambazo zinaandaliwa akizitaja Tuzo za Filamu zinazoandaliwa na Bodi ya filamu,Tuzo za Muziki chini ya Uongozi wa Baraza la Sanaa taifa(BASATA) lakini kumekuwepo changamoto ya eneo la Tamthilia kutopewa Nafasi kubwa zaidi.

Mjata amesema Tuzo hizo za Filamu zitashirikisha Watayarishaji, Wasanii,Wadau wengine kutoka nchi mbalimbali duniani.

"Tunapenda Kuishukuru Wizara ya Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambapo tulifanya kikao nao nakuomba mambo kadhaa yakiwemo kutafuta fursa kama programu za Kubadilishana uzoefu katika nchi mbalimbali ikiwemo Uturuki, noChina,Japan,Marekani, India,Pakistan, Ufaransa, Ujerumani, Ufilipino na Uingereza."

Nae Mwakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Idara ya Diplomasia na Uchumi Maryam Vuai amesema Mambo yaliyotumwa na Waandaaji wa Tuzo hizo yamefika Wizarani na watahakikisha wanatoa Ushirikiano Mkubwa kupitia Sekta ya Filamu.

Vuai ameongeza kuwa Wizara inategemea kupitia tuzo hizo zitaweza kubadilishana uzoefu na Utamaduni kupitia nchi shiriki pamoja na Kukuza Lugha ya Kiswahili.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...