Skip to main content

DOYO AFANYA ZIARA ZANZIBAR APOKELEWA KWA SHANGWE NLD

 



Zanzibar.

Katibu Mkuu wa  chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, leo tarehe 11-09-2024 amewasili Visiwani Zanzibar kwa ziara ya chama cha NLD. Katika ziara hiyo, Mhe. Doyo ameambatana na viongozi mbalimbali wa chama hicho kutoka upande wa Bara na kupokelewa na baadhi ya viongozi wa chama hicho upande wa Zanzibar, akiwemo Mwenyekiti wa chama cha NLD Taifa, Mhe. Mfaume Khamis Hassan.

Mhe. Doyo na Mwenyekiti wa NLD walifanya kikao cha ndani na baadhi ya wanachama wa chama hicho upande wa Zanzibar, ambapo wote kwa pamoja walitoa mwito wa kuimarisha ujenzi wa chama na ushirikiano kati ya wanachama wa NLD kutoka Bara na Zanzibar.

Akizungumza na wanachama wa NLD, Mwenyekiti wa chama hicho Mhe. Mfaume Khamis Hassan aliwataka wanachama wa NLD nchini kumuunga mkono Mhe. Doyo ili kuleta mabadiliko ndani ya chama hicho, akimwelezea Mhe.Doyo kama mtu muadilifu na mtendaji mzuri wa kazi za chama. Mwenyekiti alisisitiza, "Hakuna chama chochote kinachoweza kumkataa mtu kama Doyo, mtu mwenye historia ya utendaji bora katika siasa za nchi hii."

Kwa upande wake, Mhe. Doyo aliwashukuru wanachama wa NLD kwa utayari wao wa kufanya kazi naye, na akawahakikishia kwamba atafanya mabadiliko makubwa ndani ya muda mfupi. Aliahidi kukifanya chama hicho kuwa miongoni mwa vyama shindani katika chaguzi zijazo. Aidha, Mhe. Doyo alimuahidi Mwenyekiti wa NLD kuwa tayari kupokea baadhi ya wanachama wanaomuunga mkono kutoka sehemu mbalimbali nchini katika harakati za muendelezo wa kuimarisha demokrasia.

"Nyuma yangu kuna kundi kubwa lililofurahishwa na sera nzuri za NLD hasa inayosisitiza uzalendo, haki, na maendeleo kwa umma," alisema Mhe Doyo, na kuimiza kwamba ukombozi wa umma utakuja chini ya mwamvuli wa NLD.

Kesho, viongozi wa chama hicho wataendelea na ziara yao ya ujenzi wa chama katika jimbo la Chaani.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...