Skip to main content

NLD YAZINDUA KAMPENI "FYEKA CCM", YATOA WITO HUU KWA TAMISEMI






Na Mwandishi wetu 

Chama Cha National League For Democracy (NLD) leo kimezindua kampeni maalum yaKkukiondoa chama Cha Mapinduzi madarakani "fyeka CCM" ambapo imelenga kuzunguka mikoa 10 ya Tanzania ikiwemo Tanga, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Singida, Dodoma na Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari na wanachama wa chama hicho, jijini Dar es Salaam kwenye makamo makuu ya chama hicho, Katibu Mkuu Doyo Hassan Doyo amesema kuwa, chama hicho kina sera nzuri ambazo zinawabeba wananchi hasa katika kuwakomboa na umaskini.

Aidha, uzinduzi wa kampeni hiyo umeenda sambamba na kuwapokea wanachama wapya kutoka chama Cha ACT -Wazalendo na ADC ambapo amesema kuwa, kupitia kampeni hiyo watategeneza  wagombea ambao wataweza kushindana kwa hoja, huku akiwataka viongozi na wanachama kutumia lugha nzuri wanapokuwa majukwaani na kufanya siasa za kistarabu.

"Siasa lazima zifanyike katika mazingira yanayoheshimika ..wanasiasa tuheshimiane .. wanasiasa tusifanye kiburi kwa viongozi ambao wako madarakani," Nakuongeza kuwa" kwa uelewa wangu siasa ni tunu inayosogeza  maendeleo kwa wananchi "alisisitiza Doyo 

Ameongeza "juzi tunasikia kuna kongamano lilifanyika nchini la wanawake wanaosadikiwa kuwa ni wanachama wa (CHADEMA) wanasema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ni muuaji maneno haya katika siasa sio mazuri tena yenye tafsiri mbaya  kwenda kumtuhumu kiongozi wa nchi ni muuaji ni kuikosea siasa za Tanzania na wananchi awawezi kuendeshwa kwa siasa za namna hiyo "amesema Doyo

Aidha amesema Chama cha NLD kinaamimi katika itikadi ya uhuru ambao una mipaka, hivyo mtu anapopewa uhuru asizungumze maneno ya kumdhalilisha mtu wala kumtuka ni kinyume cha sheria, hivyo wanapofanya siasa lazima wajue uhuru walionao pia una mipaka yake, hivyo wazumgumze maneno yenye staha.

"Chama Cha NLD, sisi tunajibu Kwa hoja, juzi Rais Dkt Samia aliwahutubia wanachama wake na kumwambia hajaona mbadala wa chama cha kushika dola, sasa sisi tunajibu chama chetu kinakuja kuonesha njia, ndio chama mbadala kinachokwenda kushika dola kwani tunasera na itikadi nzuri NLD inaamini katika haki na uzalendo "amesema Doyo

Katika hatua nyengine, ameiomba Ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za mtaa (TAMISEMI) kusogeza mbele Uchaguzi wa Serikali za mitaa kwani muda wa kujiandaa uliowekwa ni mdogo, hawawezi kukamilisha ndani ya siku sita.

"Tunaiomba TAMISEMI irekebishe ratiba ya Uchaguzi wa Serikali za mitaa siku za mchakato ziongezwe ili vyama vya siasa viweze kujipanga vizuri, na kushiriki kikamilifu ikiwa ni pamoja na kusimamisha wagombea na kujindikisha  na kupiga kura"amesema Do you.


Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...