Skip to main content

PAMBANO LA NOCK OUT YA MAMA KUPIGWA OCT 5, DAR

 




Na Mwandishi wetu,Dar 

Wadau na mashabiki wa boxing wajiandae kupokea burudani ya kutosha kutoka kwenye pambano la kimataifa la Knockout ya mama litakalopigwa katika viwanja vya magomeni sokoni jijini Dar es Salaam Ock 5 mwaka huu.

Pambano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Mafia Boxing Promotion ambapo pambano hilo litawakutanisha mabondia mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi akiweno Ibrahim Mafia kutoka Tanzania na Said Chino .



Akizungumzia kuhusu maandalizi ya pambano hilo mbele ya waandishi wa habari mapema leo Septemba 26,2024 Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo Anthony Nurgazi amesema kwamba pambano hilo litawakutanisha mabondia Ibrahim Mafia Tz na Said Chino katika kuwania mkanada wa WBC.

"Kama ilivyo katika Mchezo wa mpira wa miguu,Rais Dkt Samia amekua akitoa zawadi ya fedha kwa kila Gori linalofungwa katika mechi za Kimataifa ili kuleta motisha kwa wachezaji,nasisi huku atujakaa mbali tumeamua kuja na pambano hili (Nockout ya Mama) mshindi atapata milioni kumi kama bonasi" amesema Nurgazi



Amesema kuwa pambano hilo la kimataifa litafanyika katika ukumbi wa City Centre Hall Magomeni, pamoja na mambo mengine, licha ya kutoa burudani limelenga kuwaenua mabondia watanzania kujulikana na kufanya kazi zenye kiwango ili waweze kufikia ndoto zao.

Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, Bondia Ibrahim Mafia Tz amesema kwamba amejiandaa vya kutosha na anaendelea kujiandaa vizuri ili aweze kukabiliana na mpinzani wake sambamba na kushinda pambano hilo.



"Mashabiki wa boxing musiwe na wasiwasi , nimejiandaa vya kutosha na naendelea kujiandaa kupigana na mpinzani wangu nitahakikisha mashabiki mutafurahia burudani hii wasiwe na wasiwsi ,nipo vizuri nawakaribisha wajitokeze kwa wingi kuja kushuhudia pambano siku hiyo" amesema.

Kwa upande wa bondia Said Chino amesema kuwa yupo tayari kupigana kwenye pambano hilo nakwamba kwa sasa anaendelea kujifua ili kuweza kumshinda mpinzani wake, ambapo ameahidi kushinda kwenye pambano hilo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...