Skip to main content

UJENZI WA OFISI YA WAKALA WA VIPIMO KUKAMILIKA JANUARI 2025

 




Na Veronica Simba, WMA Dodoma

Imeelezwa kuwa ujenzi unaoendelea wa Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo (WMA) unatarajiwa kukamilika Januari 2025.

Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa WMA, Karim Zuberi amemweleza hayo Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya aliyefanya ziara kujionea maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo eneo la Medeli jijini Dodoma, Septemba 27, 2024.

Akiwasilisha taarifa fupi kwa Katibu Tawala, Zuberi amesema Mkandarasi amebakiwa na wiki 14 kukamilisha Mradi huo wa miaka miwili na nusu wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni sita za kitanzania (TZS 6.17)

“Kutokana na kazi iliyofanyika hadi sasa, Mkandarasi ameshalipwa shilingi bilioni 3.8 sawa na asilimia 61.6 ambapo Mradi umefikia asilimia 79.4”

Aidha, Zuberi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuidhinisha bajeti ya mapato ya ndani katika kutekeleza Mradi huo.

Ametaja miongoni mwa manufaa yatakayopatikana baada ya jengo hilo kukamilika kuwa ni pamoja na kuongeza morali ya kazi kwa wafanyakazi wa WMA kutokana na uwepo wa mazingira mazuri ya Ofisi.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mmuya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya WMA Mkoa wa Dodoma, pamoja na kupongeza kazi nzuri inayoendelea kufanyika, amemsisitiza Mkandarasi pamoja na Mshauri Elekezi kuzingatia viwango vya ujenzi wa majengo ya Serikali.

Akifafanua, Mmuya amesema pamoja na mambo mengine, ni muhimu kuhakikisha miundombinu mbalimbali ya jengo hilo inakuwa wezeshi kwa watu wenye ulemavu.

Tangu kuanza kwa ujenzi wa Jengo la Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo Julai 2, 2022, viongozi mbalimbali wametembelea kukagua maendeleo yake akiwemo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ambaye aliweka Jiwe la Msingi Februari 6, 2024.

Wengine ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo aliyetembelea na kukagua Mradi Julai 17, 2024, aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji (Agosti 24, 2023) pamoja na Katibu Mkuu Wizara hiyo, Dkt. Hashil Abdallah (Januari 3, 2023)

Mradi wa Ujenzi wa Ofisi Kuu ya Wakala wa Vipimo unasimamiwa na Mshauri Elekezi MUST Consultancy Bureau Limited na kutekelezwa na Mkandarasi kampuni ya Mohammedi Builders Limited.

Ofisi za WMA zipo katika mikoa yote Tanzania Bara ambapo jukumu lake kuu ni kuzilinda pande mbili yaani mlaji na muuzaji wa bidhaa na huduma kupitia matumizi sahihi ya vipimo

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...