Skip to main content

WAZIRI JAFO: WIZI WA KUCHEZEA VIPIMO NI KOSA KISHERIA



 Na WMA, Mwanza

Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo amehimiza wananchi jijini Mwanza kuzingatia matumizi sahihi ya vipimo kila mara wanapofanya manunuzi na kuuza bidhaa mbalimbali.

Aliyasema hayo Septemba 11, 2024 wakati akifungua rasmi Maonesho ya 19 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayofanyika katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.

 "Wizi wa kuchezea vipimo ni kosa kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo Sura Na. 340 na hata vitabu vya dini vinakataza wizi wa vipimo," alisisitiza.

Katika hatua nyingine, akizungumzia ushiriki wa Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho hayo, Afisa Vipimo Mwandamizi Mkoa wa Mwanza, Lazaro Joram alisema ni mwendelezo wa utoaji elimu kwa umma kuhusu matumizi sahihi ya vipimo kwa wafanyabiashara waliopo ndani ya Mkoa wa Mwanza pamoja na nchi jirani.

"WMA tunatumia Maonesho haya ili kuwawezesha wadau wetu kutambua majukumu yetu, kueleza umuhimu wa kuhakiki na kutumia vipimo sahihi na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya matumizi ya vipimo pamoja na kuendelea kuwaelimisha kuhusu aina za vipimo vinavyopaswa kutumika katika biashara."

Joram aliwakaribisha wananchi kutembelea Banda la WMA ili kufahamu aina za mizani wanazoweza kutumia katika sekta za kilimo, uvuvi, biashara na usafirishaji.

“Tunazo aina nyingi za mizani lakini siyo kila mzani unaruhusiwa kutumika katika biashara au katika sekta ya kilimo hivyo ukitembelea Banda letu tutakupa elimu ya kutambua mizani sahihi iliyohakikiwa pamoja na kutambua alama zinazowekwa katika vipimo vilivyo hakikiwa,” alisema.

Akidadavua kuhusu elimu inayotolewa kwa wananchi wanaotembelea Banda la WMA, Joram alisema eneo mojawapo ni kuhusu namna sahihi ya ufungashaji wa mazao ya shamba ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Vipimo mazao yote yanatakiwa kufungashwa kwa uzito usiozidi kilogramu mia moja (100 kg) na endapo mkulima atafungasha mazao kwa uzito zaidi ya uliotajwa kisheria atakuwa amefungasha Lumbesa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

“Kwa sasa tafsiri ya lumbesa ni uzito unaozidi kilo mia moja (100 kg) tofauti na awali ambapo ilikuwa inatafsiriwa kama kuongeza kifungashio juu ya gunia hivyo tunawahimiza wakulima kutumia mizani ili kujua uzito wa mazao wanayofungasha,” alisisitiza.

Akieleza zaidi, alisema kuwa, Kanda ya Ziwa kuna mazao ya kimkakati aina mbili ambayo ni Pamba na Kahawa ambapo jukumu la WMA ni kuhakiki mizani zote zinazotarajiwa kutumika kwenye ununuzi wa mazao hayo kabla ya msimu kuanza na baada ya kufanya uhakiki mizani iliyo sahihi huruhusiwa kutumika katika ununuzi wa mazao hayo. 

Vilevile, alisema wakati wa ununuzi, WMA hufanya kaguzi za kushtukiza katika Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) ili kujiridhisha kama mizani zinatumika kwa usahihi kama zilivyo hakikiwa ili kuwalinda wakulima.

Pamoja na majukumu mengine, WMA pia ina jukumu la kusimamia usahihi wa vipimo kwenye sekta ya usafirishaji ambao ni pamoja na usafiri wa anga, barabara na usafiri wa majini kwa kuhakikisha mizani zinazotumika ziko sahihi na zimehakikiwa ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza ikiwemo kubeba mizigo yenye uzito mkubwa ambayo inaweza kusababisha vyombo hivyo kuanguka na miundombinu kuharibika.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WMA anayeshiriki Maonesho hayo, Paulus Oluochi alitoa wito kwa wananchi kutembelea Banda la WMA ili kujifunza kuhusu matumizi sahihi ya vipimo lakini pia kuwasilisha changamoto mbalimbali kama zipo ili ziweze kupatiwa ufumbuzi. 

Alisema endapo mwananchi yupo mbali, anaweza kuwasiliana na WMA kupitia nambari isiyo na malipo 0800 110097.

Maonesho hayo ya 19 ya Biashara ya Afrika Mashariki yanatarajiwa kufikia tamati Septemba 15, 2024.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...