Skip to main content

HUU NDIO USHAURI WA TMA KWA SEKTA HIZI ...



Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na Wakulima, Wafugaji, Mamlaka za wanyamapori , Mamlaka za maji na Afya waendelee kutafuta, kupata na kuzingatia ushauri wa wataalamu katika sekta husika ili kujiepusha na athari za mvua zinaponyesha.

Ushauri huo umetolewa leo Oktoba 31,2024 Jijini Dar es salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ambaye pia  Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang'a wakati akitoa taarifa ya mwelekeo wa mvua za Msimu wa Novemba, 2024 hadi Aprili 2025.

Amesema kuwa, mvua za msimu ni mahususi katika maeneo ya Magharibi mwa nchi Kanda ya kati, Nyanda za juu kusini Magharibi kusini, ukanda wa  Pwani ya kusini pamoja na maeneo ya kusini mwa mkoa wa Morogoro ambapo maeneo hayo yanapata msimu mmoja kwa mwaka.

Aidha, kutokana na mifumo ya hali ya hewa, mvua za wastani hadi chini wastani zinatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Songwe, Singida, na Dodoma, huku juu ya wastani zikitarajiwa katika mikoa ya Njombe,Ruvuma,Mtwara,maeneo ya kusini na Magharibi mwa mkoa wa Lindi, kusini mwa mikoa ya Mbeya, Iringa na Morogoro.

"Mvua nyingi zinatarajiwa katika kipindi Cha nusu ya pili ya msimu kuanzia mwezi February hadi April kwa mwaka 2025, ikilinganishwa na Nusu ya kwanza mwezi Novemba 2024 hadi Januari 2025"

Aidha, vipindi vifupi vya mvua kubwa vinaweza kusababisha kutuama kwa maji, kuongeza mtiririko na kusababisha mafuriko ambayo yanaweza kupelekea uharibifu wa miundombinu na tishio la usalama wa maisha na mali, hivyo mamlaka za miji zinashauriwa kuboresha na kuimarisha mifumo ya maji taka na safi mijini ili kupunguza athari za mafuriko.

Hata hivyo, amesema jamii imeshauriwa kutibu maji ya kunywa, kuzuia na kuharibu mazalia ya mbu, kuzingatia matumizi sahihi ya vyoo, kuendeleza tabia ya kunawa mikono Kwa sabuni na maji tiririka na kudumisha usafi wa mazingira kwa maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani.

Katika msimu huo wa mvua kubwa kutokea na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi ambayo yanaweza kusababisha uharibifu wa miundombinu mazingira kupoteza mali na madhara kwa binadamu, hivyo idara ya Menejment ya msaada nchini inashauriwa kuendelea kuratibu utekelezaji wa mipango itakayosaidia kupunguza madhara yatakayojitokeza.

Hata hivyo, wadau WA sekta binafsi wanashauriwa kushirikiana na wataalam mbalimbali ikiwemo watalaam wa Hali ya hewa ili kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza, Taasisi za benk na bima zinashauriwa na kutoa huduma mahususi Kwa wadau ili kujenga ustahamilivu katika biashara.

Katika hatua nyingine Kaimu Mkurugenzi mkuu huyo wa TMA amesema kuwa Mifugo na Uvuvi katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani, wafugaji na wavuvi wanatarajiwa kunufaika na upatikanaji wa malisho, maji na chakula cha samaki. 

Hata hivyo amesema milipuko ya magonjwa ya mifugo kama vile homa ya bonde la ufa, ugonjwa wa miguu na midomo, na kuzaliana kwa wadudu wadhurifu kunaweza kujitokeza. 

Pia amesema upungufu wa mvua hasa katika nusu ya kwanza ya msimu (Novemba, 2024 hadi Januari, 2025) unatarajiwa kuathiri upatikanaji wa maji na malisho ya mifugo na kusababisha migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.

"Wafugaji wanashauriwa kuweka mipango mizuri ya matumizi na uhifadhi wa maji na vyakula vya mifugo,wafugaji na wavuvi wanashauriwa kutumia taarifa za utabiri wa hali ya hewa na kuzingatia ushauri unaotolewa na maofisa ugani ili kupunguza athari zinazoweza kutokea na kunufaika na hali ya hewa inayotarajiwa."amesema Dr.Chang'a

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...