Skip to main content

SERIKALI YAAHIDI KUWEKA MAZINGIRA MAZURI KWA WABUNIFU WA MAJENGO



Na Mwandishi wetu 

Serikali imesema ipo kwenye mchakato wa kufanyia maboresho sera ya ujenzi ili kutengeneza sheria ya ujenzi itakayosidia  wataalamu wa wabunifu majengo na wakadiriaji ujenzi AQRB kufikia matamanio ya kukuza sekta ya ujenzi kutokana na mabadiliko ya teknolojia yanayoenda kwa kasi duniani.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Edward Mpogolo wakati akimuwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Mashaka Biteko kwenye ufunguzi wa Mkutano wa  5 wa Bodi ya wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji Majenzi ambapo unafanyika kwa siku mbili.



Amesema kuwa, mkutano huo uwapeleke kwenye tafakuri ya kuangalia changamoto walizopitia kwa kipindi cha miaka 5 na kuzifanyia kazi katika maboresho ili kuweza kupiga hatua zaidi kama Taifa na kwenda mbele kwenye ubunifu zaidi.

Ameongeza kuwa, licha ya changamoto kubwa wanazozipitia lakini pia wameweza kupata mafanikio makubwa ikiwemo kusajili wabunifu 1586 huku 33 ndio wakitoka nje.



Aidha, ametoa wito kwa Wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji  Majenzi (AQRB)wametakiwa kuwa wazalendo ili kuhakikisha wanatekeleza kwa wakati miradi ya ujenzi wanayopatiwa na Serikali au sekta binafsi.

Hata hivyo, amesema kuwa baadhi ya wataalamu wa ubunifu wa majengo na ukadiriaji majenzi wamekua wakiangalia maisha yao binafsi kwa ajili ya kujipatia fedha kwa muda mfupi huku suala la weledi kazini likiwa limewekwa pembeni hali ambayo inasababisha majengo kuwa chini ya kiwango.



"Jitihada zinazopatikana katika sekta ya ujenzi inatokana na nyinyi wataalamu wa ubunifu wa Majengo na ukadiriaji Majenzi,ukiona mafanikio yaliyopo kwa sasa yanatokana na nyinyi,hivyo kwa niaba ya serikali  nawaomba sana muwe Wazalendo ili tumuunge mkono Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan" amesema DC Mpogolo.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TBA Dkt Daudi Kondoro amewapongeza watoa mada ambao wamechaguliwa katika mkutano huo kutokana na uzoefu wao ambapo watawapatia madam zenye welezi wahitimu ambapo watapatiwa mafunzo hayo.



Aidha, amesema watendaji wa wizara wataendelea kusimamisha sekta ya wataalamu wa ubunifu wa Majengo na Wakadiriaji Majenzi ili waweze kua na weledi katika kazi zao.

"Wizara ya ujenzi itatenga fedha kwa ajili ya kuendelea kutoa mafunzo wataalamu 180 Kila Mwaka ambao wanahusika na bunifu wa Majengo na ukadiriaji Majenzi,ili waweze kuwa na uelewa Moana katika taaluma yao" amesema Dkt.Kondoro.

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi wa wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji majenzi (AQRB) Dkt Ludigija Bulamile amesema kuwa miongoni mwa mada ambazo zitakazojadiliwa ni pamoja na mafunzo ya ubunifu wa kijani ambapo yamedhaminiwa na Wold benki (WB) .

Pamoja na muhtasari wa mpango mkakati wa wizara kuwawezesha wazawa ambapo makampuni ya ndani yachukue nafasi kubwa katika kusimamia miradi mikubwa inayotolewa na Serikali .

 "Utafiti wa vifaa vya ujenzi, mfumo wa ununuzi katika sekta ya ujenzi"

Mkutano huo wa tano wa Bodi ya wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji Majenzi( AQRB) umeenda sambamba na mahafali ya kwanza ya wahitimu wa mafunzo ya taaluma ya wabunifu Majengo na wadiriaji Majenzi ,ambapo zaidi ya wahitimu 130 wamepewa vyeti pamoja na muongozo utakaowasaidia kufanyia kazi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...