Skip to main content

WADAU WA KUPINGA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI WAKETI DAR, CDF, TAWLA WATOA NENO




Na Mwandishi wetu Dar

IMEELEZWA kuwa katika harakati za kumkwamua mtoto wa kike kuweza kupiga hatua kimaendeleo na kuzifikia ndoto zake, Serikali inajukumu kubwa la kutengeza mazingira salama na wezeshi ili kuhakikisha mtoto wa kike anapata haki sawa ikiwemo kuzuia ndoa za utotoni na kuruhusiwa kurudi mashuleni.

Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF) kwa kushirikiana na Chama Cha wanasheria wanawake Tanzania (TAWLA) wakisapotiwa na Shirika la Equality Now leo limewakutanisha wadau mbalimbali wa maendeleo ya Jamii ili kujadili sheria ya ndoa hasa kifungu cha 13 na 17 kinachoruhusu mtoto wa kike kuolewa chini ya umri wa miaka 18.

Katika mkutano huo wa mashirika yasiyo ya kiserikali CSO, wadau hao wataweza kujadili nini kifanyike katika mapendekezo kadhaa yaliotolewa na Mahakama kwenda kwa Serikali ikitaka sheria ya ndoa kupitia kifungu cha 13 na 17 ibadilishwe ili kumlinda mtoto wa kike asiweze kuolewa katika umri mdogo pamoja na kumlinda na madhara ya ndoa za utotoni.

Koshuma Mtengeti ni Mkurugenzi wa Jukwaa la Utu wa Mtoto CDF ameeleza kuwa pamoja na mambo mengine wataangalia sera ya kumrudisha mtoto shuleni ambae amebeba mimba akiwa shuleni, ambapo watajadili kwa pamoja ni kwa namna gani watoto hao wataweza kusaidiwa ili wapate haki ya elimu. 



Akizungumzia suala la ukatili wa kingono ameeleza kuwa, takwimu zinaonesha asimilia 33 ya watoto wa kike wanapitia ukatili wa kingono ikiwemo mimba za utotoni na ndoa za utotoni ikilinganishwa na silimia 17 kwa watoto wa kiume .

Aidha, amesema katika maboresho ya ndoa, jambo la kwanza linaloonekana ni utayari wa kisiasa, mila na desturi ambapo hayo yote ni ya kuyafanyia kazi ili kumlinda mtoto wa kike, huku unyanyapaa ukishika kasi Pindi watoto hao wanaporudi mashuleni, pia hakuna mazingira rafiki ya wao kurudi mashuleni.

Kamati ya wataalam ya watoto wa Afrika inatoa mapendekezo kwa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya wanafunzi waliopata mimba wakiwa mashuleni ambapo inataka waruhusiwe kusoma bila kikwazo chochote.



Mkurugenzi wa Chama cha wanasheria wanawake Tanzania (TAWLA) na Mwenyekiti wa Mtandao wa kupinga ndoa za utotoni Itike Mwakimbile ameeleza wamekutana wao kama wadau kuangalia sera, mifumo na sheria zake zinazofanya kazi,ambapo ni kwa namna gani zinaweza ikabana sheria hizo ili kuzuia ndoa na mimba za utotoni.

Ameeleza kuwa sheria hizo zinaruhusu mtoto akiwa na miaka kati ya 14 na 15 kuolewa hivyo, wanafanya uchechemuzi kuangalia ni kwa namna gani sheria hizo zinaweza kuleta mabadiliko kutoka miaka hiyo hadi 18, ambapo kwa umoja wao watashirikiana kupaza sauti ili jamii kutambua madhara ya mimba za utotoni kwani madhara yake ni makubwa.

Rose Elisante ni Afisa program kutoka Shirika la Haki Elimu amesema licha ya kutoa semina kwa wadau kuhusu kuwa na uwelewa wakupokea watoto waliocha shuleni kutokana na kupata mimba lakini bado imeonekana suala hilo limegubikwa na changamoto kadhaa.



Muongozo uliotolewa juu wanafunzi walioapata mimba kurudi mashuleni umewapa nafasi maafisa elimu na walimu kuwapokea wanafunzi wanaorejea mashuleni lakini hali ya wanafunzi hao kunyanyapaliwa wanafunzi wenzao, kuitwa majina masiyofaa, mlolongo mrefu wa kuwataka wazazi kupitia wizarani imekua ni kikwazo cha baadhi yao kujikuta wanaacha tena shule.

"Hata zile sababu zilizowafanya wakatishe shule bado hazijafanyiwa marekebisho ikiwemo kutembea umbali mrefu, kukosa sodo kwa wanafunzi wa kike mashuleni, sisi kama wadau tunaendelea kutoa elimuna hamasa Kwa walimu na wanafunzikuweza kuwapokea ili waweze kusoma"

Mdau kutoka maendeleo ya Jamii ambae alishiriki katika mkutano huo Rogathe Loakaki amesema suala ya mtoto wa kike ni ajenda ya watu wote kwani wanatambua changamoto ni kubwa hivyo wao kama wadau watahakikisha maadhimio yatakayofikiwa wanayafanyia kazi ili kusukuma gurudumu hilo ili kumkwamua mtoto wa kike katika nyanja zote.





Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...