Skip to main content

KUANZIA JANUARI 2025, VIVUKO VITAKUWA VINASUBIRIA ABIRIA, SEA TAX KUONGEZWA DAR: BASHUNGWA







Na Mwandishi wetu, Dar 

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) kwa kushirikiana Kampuni ya Azam Marine zinaendelea kuboresha utoaji wa huduma za usafiri wa vivuko katika eneo la Magogoni – Kigamboni jijini Dar es Salaam ambapo kufikia mwezi Januari 2025 vitaongezwa vivuko vidogo (sea tax) kufikia sita (6) ambapo ushirikiano huo utaondoa changamoto kwa wananchi kusubiri vivuko kwa muda mrefu. 

Bashungwa ameeleza hayo leo Novemba 19, 2024 Dar es salaam wakati akikagua huduma za usafiri wa vivuko ambapo ameeleza kutokana na changamoto iliyopo sasa, kuanzia kesho (Novemba 20,2024) Azam Marine kwa kutumia sea tax itaongeza muda wa kutoa huduma kulingana na ilivyokuwa awali ili kupunguza msongamano wakati wa asubuhi na jioni. 



“Nimeelekeza  kufika Disemba 31, 2024 majengo ya kisasa ya abiria yawe yamekamilika na tuingie mwaka mpya wa 2025 tukiwa na Sea tax za Azam sita, hilo lina maanisha kuanzia Januari 01, 2025 vivuko vitakuwa vinasubiria abiria badala ya abiria kusubiria vivuko ambapo mwananchi atasubiri kivuko kwa dakika zisizozidi 3”, amesema Bashungwa. 

Bashungwa ameeleza kuwa uboreshaji wa utoaji wa huduma za usafiri wa vivuko unaenda sambamba na ujenzi wa majengo ya abiria ya kisasa na uboreshaji wa majengo yaliyokuwepo ambapo ameagiza kazi hiyo ikamilike ifikapo Disemba 31, 2024.


Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inaendelea na mazungumzo na kampuni ya Azam Marine kwa ajili ya kuboresha huduma ya usafiri wa vivuko kwa wananchi wa Mafia ili kurahisisha huduma za usafiri na usafirishaji na kuchochea shughuli ya Utalii na Uchumi kwa wananchi wa mkoa wa Pwani. 

Katika hatua nyingine, Bashungwa amekagua ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV Kigamboni katika karakana ya Songoro Marine ambapo amebainisha kuwa Serikali tayari imemlipa kiasi cha Shilingi Bilioni 5.6 kwa ajili ya ukarabati wa vivuko mbalimbali nchini, hivyo amemtaka Mkandarasi huyo kukamilisha ukarabati kwa kivuko hicho kwa wakati ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi wa Kigamboni.


Wakati huo, Bashungwa ametoa onyo kali kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao katika njia za vivuko na kupelekea nyavu kunasa kwenye vivuko na kusababisha hitilafu ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Lazaro Kilahala ameeleza ushirikiano na kampuni ya Azam Marine umeongeza utoaji  huduma ya usafirishaji kwa wananchi wakati ukarabati wa Vivuko vya MV Kigamboni na MV Magogoni ukiendelea na kufafanua kuwa changamoto iliyojitokeza imetokana na sea tax moja kupata hitilafu.


Naye, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni Azam Marine, Abubakar Aziz ameeleza kuwa mpaka sasa ujenzi wa majengo ya abiria kwa upande wa Magogoni umefikia asilimia 70 na upande wa Kigamboni umefikia asilimia 60, majengo hayo yatahusisha ofisi za mawakala wa mauzo ya tiketi kwa njia ya kielektroniki.



Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...