Skip to main content

WAKILI MWABUKUSI AFUNGUKA KUTUPILIWA MBALI MAOMBI YA MDUDE.







Na Mwandishi wetu, Dar 

Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya mawakili wa upande wa utetezi kutaka mwanaharakati Mdude Nyagali afikishwe mahakamani kwa madai kuwa kiapo kinzani hakijathibitisha kujeruhiwa na kushikiliwa kinyume cha sheria kwa mwanaharakati huyo.

Mawakili Boniface Mwabukusi na mwenzake Philip Mwakilima, walieleza hoja za mwanaharakati Mdude Nyagali Mpaluka kushikiliwa kinyume cha sheria na kwamba mpaka sasa bado yuko mikononi mwa Polisi hivyo pia walikuwa wakiiomba mahakama iamuru mwanaharakati huyo afikishwe mahakamani.

Hata hivyo Jaji wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Mbeya aliyekuwa akisikiliza maombi hayo Musa Pomo ametupilia mbali maombi hayo akisema upande wa waleta maombi (Wakili Mwabukusi na Mwakilima) hawajathibitisha kuwa Mdude Nyagali alipigwa wala kujeruhiwa jambo ambalo linaelezwa na mawakili wa utetezi kuwa halikuhitajika na upande wowote mbele ya Mahakama na kama kungehitajika uthibitisho wa vielelezo wangewasilisha ikiwemo mlalamikaji (Mdude Nyagali) kufika mahakamani kueleza madhira yaliyomkuta.

Kwa upande wa mashtaka shauri hilo lilikuwa likiendeshwa na wakili Lodgard Eliaman na wakili Dominic Mushi huku waleta maombi wakiwa ni wakili Boniface Anyisile Kajunjumele Mwabukusi na mwenzake Philip Mwakilima ambapo akizungumza baada ya kutupiliwa mbali kwa shauri hilo Wakili Mwabukusi amesema hawakubaliani na maamuzi ya Mahakama kuu hivyo watajadiliana kuona namna bora ya kufanya kwasababu wanaamini Mdude Nyagali alipigwa na anashikiliwa kinyume cha sheria.

Itakumbukwa kwamba mwanaharakati na mwanachama wa CHADEMA Mdude Nyagali Mpaluka alikamatwa Novemba 22, 2024 huko Mbozi mkoani Songwe pamoja na uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa waliokuwa kwenye mikutano ya kampeni za uchaguzi wa Serikali za mitaa akituhumiwa kwa makosa kadhaa ikiwemo kutoa lugha za matusi na kujeruhi ambapo tangu kukamatwa kwake aliendelea kusalia mikononi mwa Polisi hadi tunakwenda mitamboni jumatatu hii hivyo mawakili Boniface Mwabukusi na Philip Mwakilima wanaishinikiza mahakama iwaamuru wahusika kumfikisha mahakamani mwanaharakati Mdude Nyagali ikiwa ana kosa lolote badala ya kuendelea kumshikilia jambo linalokinzana na sheria za mwenendo wa makosa ya jinai.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...