Skip to main content

BENKI KUU YANUNUA TANI 2.6 ZA DHAHABU INAYOCHIMBWA NCHINI – WAZIRI MAVUNDE





BoT yanunua dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 570

Asisitiza dhamira ya Tanzania kuwa miongoni mwa mataifa 10 yenye hifadhi kubwa ya dhahabu Afrika

Abainisha kuongezeka kwa mapato yatokanayo na madini ya dhahabu

Dodoma

Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amebainisha kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imenunua tani 2.6 za dhahabu inayochimbwa na kusafishwa hapa nchini ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukabiliana na changamoto ya upungufu wa fedha za kigeni, kuboresha akiba ya fedha za kigeni, na kuimarisha thamani ya shilingi ya Tanzania.

Amesema hayo leo Januari 22, 2024, jijini Dodoma, wakati akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, taarifa inayohusu utendaji wa viwanda vya kusafisha dhahabu nchini kwa kipindi cha Machi hadi Desemba 2024 pamoja na mwenendo wa ununuzi wa dhahabu unaotekelezwa na BoT.

Mwenendo wa Ununuzi wa Dhahabu BoT

Kwa mujibu wa Waziri Mavunde, tarehe 1 Oktoba 2024, Tume ya Madini ilitoa tangazo linalowataka wachimbaji na wafanyabiashara wa dhahabu kutekeleza takwa la Kifungu cha 59 cha Sheria ya Madini Sura 123, ambalo linawataka kutenga asilimia 20 ya dhahabu na kuiuzia BoT kupitia viwanda vya usafishaji vilivyoidhinishwa.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, Tangu kutolewa kwa tangazo hilo hadi Januari 21, 2025, BoT imefanikiwa kununua tani 2.6 za dhahabu kutoka kwa wachimbaji wa kati, wachimbaji wadogo, na wafanyabiashara wa dhahabu. Thamani ya dhahabu hiyo ni zaidi ya shilingi bilioni 570 kwa mujibu wa bei ya soko la dunia ya tarehe 22 Januari 2025” amesema Mhe. Mavunde. 

Halikadhalika, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa, kupitia mpango huo wa BoT, lengo la Serikali ni kuifanya Tanzania kuwa moja ya mataifa 10 yenye hifadhi kubwa ya dhahabu barani Afrika kwa ustawi wa taifa.

Ongezeko la Mapato ya Serikali

Kwa upande wa mapato, Waziri Mavunde amebainisha kuwa, mwenendo wa ukusanyaji wa mrabaha kwa upande wa madini ya dhahabu umeendelea kuimarika na kwamba kuanzia Julai 1, 2024 hadi Desemba 31, 2024, Serikali iliingiza shilingi bilioni 400.22 kutokana na mauzo ya kilogramu 34,826.75 za dhahabu, ikiwa ni ongezeko la asilimia 5.55 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2023, ambapo kilogramu 32,995.54 ziliuzwa na Serikali kupata shilingi bilioni 278.86.

Maendeleo ya Kiwanda cha Kusafisha Makinikia – Kahama

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde aligusia maendeleo ya Kiwanda cha Kusafisha Makinikia cha Tembo Nickel Refining Limited, kitakachojengwa Kahama, mkoani Shinyanga katika eneo ambalo awali lilikuwa likitumiwa na Mgodi wa Buzwagi, ambao umesitisha shughuli za uzalishaji wa dhahabu.

Amefafanua kuwa mradi wa Kiwanda hicho ni moja ya miradi machache barani Afrika inayozalisha bidhaa iliyotayari kwa matumizi, hivyo unatarajiwa kuleta tija kubwa kwa uchumi wa nchi, sambamba na kuimarisha Mchango wa Sekta ya Madini.

Faida za Mpango wa BoT

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dkt. Mathayo David, amepongeza juhudi hizo na kueleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuimarisha shilingi ya Tanzania, kuimarisha akiba ya dhahabu, na kuiweka nchi katika orodha ya mataifa yenye hifadhi kubwa ya dhahabu ulimwenguni.

Juhudi hizo ni sehemu ya mikakati ya Serikali kupitia Wizara ya Madini kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inatoa mchango mkubwa zaidi kwa uchumi wa Taifa na ustawi wa wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...