Skip to main content

UWOYA AJA KIVINGINE, AMPA HEKO RAIS DKT SAMIA "KILIMO KINALIPA"





Mwenyekiti wa mradi wa Kilimo Jembe ni Mama Msanii wa bongo movie Iren Uwoya amesema  Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassani na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe katika kipindi cha miaka minne  kumekuwa na mageuzi makubwa sana kwenye sekta ya Kilimo chini ya .

Kauli hiyo ameitoa leo Janiari 26, 2024 jijini Dar es Salaam katika hafla fupi ya  kutambulisha mradi huo wa Jembe ni Mama katika mkutano na waandishi wa habari amesema kuwa Serikali imeota ruzuku ya mbolea, pembejeo,mikopo, na kuwatafutia masoko wakulima ili wauze mazao ya Kwa bei nzuri bila ya kupata hasara hivyo hilo ni jambo la kipekee.

 " Mradi huu wa Jembe ni Mama wataungana kufanya ziara nchi mzima Kwa wanawake wote wanafanyia Kilimo Kwa kuwatia moyo wasikate tamaa kwani Kilimo ni uti wa mgongo wa mtanzania na husaidia kusomesha watoto kulisha familia kujenga mkazi bora wanawake tutambee sisi ni nguzo muhimu Kwa familia Kilimo hakimtupi mtu " amesema Irene Uwoya.

Irene Uwoya Amesema  2018 aliamua rasmi kujiunga na Kilimo 2018 Kwa kuanzia kulima Mkoani Tanga na Mbeya zao la mpinga na Tangawizi licha ya kuwa na shughuli nyingine lakini aliona  mafanikio na alifanya tafiti kuhusu wanawake wanaojishaghulisha na Kilimo na kugundua walikuwa wanakumbana na changamoto ya kulim Kilimo duni hivyo alifanya mahojiano nao na kuwapatia elimu namna na kulima Kilimo cha kisasa .

Aidha amesema kuwa katika kuhakikisha Iren Uwoya anaisaidia sekta ya Kilimo na Serikali ya Jamuhuri wa Muungano Tanzania ameamua kufanya tamasha kubwa (Jembe ni Mama Festival) ambalo limelenga kuwainua wakulima wadogo wadogo hasa wanawake kila Mkoa watakaopita watahamasisha kuhusu Kilimo.

Hata hivyo, amesema kuwa tamasha hilo kubwa la Kilimo ambalo litalenga kutengeneza mtandao wa Kilimo siku rasmi ya wakulima wanawake Tanzania.

"Mwanamke ndie anaetumika kwenye mnyororo wa thamani wa Kilimo lakini mwanaume ndie anampangia bei baada ya kuvuna, wanaume hawashiriki kuanzia mwanzo wanakuja mwisho wa mavuno"amesema Uwoya.

"Tutaanza kuwatembelea wakulima wanawake wote nchini Tanzania wanaojishulisha na Kilimo kuwavumbua hasa wale wanafanyia Kilimo duni na kuwasaidia kwa kuwawezesha katika kilimo cha kisasa"

Ameongeza kuwa Rais DKT Samia Suluh Hassan na Waziri wa Kilimo Hussen Bashe wametengeza njia kwenye Kilimo ikiwa ni pamoja na kupata pembejeo , mikopo ya Kilimo na matumizi Tehama kwenye Kilimo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...