Skip to main content

BALOZI WA ASANTE MAMA, WAFUNGUKA YUMO SHAMSA FORD, MAFUFU, JB, KINGWENDU

 

Msanii wa filamu, Jimmy Mafufu akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kuhamia chama cha mapinduzi (CCM) mkutano uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam
Shamsa Ford aliyekuwa kada wa chadema akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kuhamia chama cha mapinduzi (CCM) mkutano uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam.
Msanii wa maigizo Single mtambile maarufu kama Richie akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari juu uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Boniventure Kabongo maarufu kama ‘Stamina" akielezea sababu za kujiunga na CCM katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hotel ya serena jijii Dar es salaam.

Dar es salaam - Wasanii wa filamu, Jimmy Mafufu na Shamsa Ford wametangaza rasmi kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa wakiwa chini ya Taasisi ya Mabalozi wa Mama na wataanza ziara nchi nzima kutangaza mafanikio ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassang yenye kaulimbiu ‘Asante Mama’.

Nyota hao ambao wameamua kujiunga CCM wakitokea katika vyama mbalimbali ikiwemo Chama Cha Demokrasia (CHADEMA) wamekiri sababu kubwa ya kuchukua uamuzi huo ni kutokana na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyofanywa na Dkt Samia ambayo inafanya taifa kukua kiuchumi.

Mafufu akizungumza amesema binafsi nimeamua kuijunga CCM baada ya kubaini kupitia Serikali ya Awamu ya Sita imefanya makubwa kwa Watanzania wakiwemo wasanii ambao wamepewa mikopo ya kuinua kazi zao.

“Licha ya kwamba mimi na Shamsha tulikuwa upinzani, mikopo hiyo inayotolewa na Rais wetu kwa wasanii haikutubagua, pia Serikali yetu imefanya mambo makubwa ikiwemo utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo kama Barabara, Bwawa la Mwalimu Nyerere, Reli ya SGR, ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato, hayo ni sehemu yaliyotukusukuma kujiunga CCM,”. Alisema Mafufu.
Alisema tangu Rais Dkt. Samia, aingie madarakani hajashindwa, ametekeleza miradi yote iliyoachwa na marehemu Rais Dkt John Magufuli, hali ambayo imefanya kutoona umuhimu wa kuwa wapinzani.

Kwa upande wake Shamsa Ford amese8 anajivunia kujiunga na CCM na nitoe wito kwa wasanii wengine ambao wako katika vyama vya upinzani kujiunga na ccm ili kuunganisha nguvu ya pamoja kutangaza miradi ya maendeleo ambayo imefanikisha kustawisha uchumi wa Tanzania.

Nae msanii wa maigizo Single mtambile maarufu kama Richie ambaye ni diwani wa CCM amesema kwa nafasi aliyonayo anaamini watatangaza, miradi yote ambayo imefanya vizuri kwa maslahi ya watanzania ili kila mmoja ajue.
.
Ameitaja miradi hiyo kuwa ni miradi ya Elimu, Afya, Usafiri wa Anga na Reli ya SGR, Bandari na mingineyo inayoifanya Tanzania kuwa mfamo wa kuigwa katika mataifa mengine.

Wasanii kutoka vyama vya upinzani ni Salum Mchoma (Chiki), Single Mtambalike ‘Richt Ritch’, Rashidi Mwishehe ‘Kingwendu’ Abdallah Mkumbila ‘Muhogo Mchungu’ na wa muziki wa kizazi kipya akiwemo Boniventure Kabongo ‘Stamina, Juma Kassim ‘Nature ‘Sir Nature’, Amani Temba ‘Capt Temba, Richard Shauri ‘Ritch One’ na wengine na lengo lao ni kutangaza miradi yote ambayo imetekelezwa chini ya Rais Samia.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...