Skip to main content

BONDIA AMIRI MATUMLA KUZICHAPA NA AMAVILA FEB 28

 


Na Mwandishi wetu 

Mkurugenzi wa Mafia Boxing Promotion Ally Zayumba amesema kuwa pambano la knock out ya mama msimu wa tatu litanogesha na mapambano 12.

Aidha katika pambano la knock out ya mama msimu wa tatu bondia Amiri Matumla atazichapa dhidi ya mpinzani wake Paul Amavila kutoka Nchini Namibia. 

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam Zayumba amesema kuwa mapambano hayo yanatarajiwa kufanyika Februari 18 Mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Zayumba amebainisha kuwa katika usiku huo pambano kuu lolitakuwa ni la Bondia Amiri Matumla ambaye atapanda ulingoni katika Ukumbi wa Magomeni Sokoni kuzichapa dhidi ya mpinzani wake kutoka Namibia, Paul Amavila.

Amebainisha kuwa Bondia Matumla katika pambano hilo atazichapa  na mpinzani wake huyo kwa mizunguko nane.

"Hili ni pambano lake la kwanza tangu ajiunge kwenye mapambano ya ngumi za kulipwa na ameahidi kufanya vizuri kwa lengo la kuanza kutengeneza rekodi nzuri katika karia yake kupitia masumbwi," amesema Zayumba.

Zayumba ameongeza kuwa mapambano mengine 11 ya utangulizi yataongozwa na mkongwe Dullah Mbabe huku baadhi ya mabondia wengine watakaopanda ulingoni wakiwa ni Oscar Richard atakayezipiga na bondia kutoka Malawi.

Wengine ni Rashid Mtange kutoka Nacoz Camp chini ya kocha Ramadhani Uhadi 'Rama Jah' atazichapa na bondia kutoka India na  wengineo.

Amebainisha kuwa mapmabo hayo lengo lake ni kunadi miradi iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Amefafanua kwamba Michezo wa ngumi katika kipindi hiki cha uongozi wa Rais Dkt Samia,  umekuwa na mafanikio makubwa hivyo ni vema watanzania wakaendelea kumuunga mkono.

Aidha, amesema kuwa ,vingilio katika usiku huo wa Knock Out ya Mama Msimu wa tatu vitakuwa ni shilingi, 50,000, sh. 20000 na 10,000.

Naye Bondia Matumla, ambaye ni mtoto wa Rashid Matumla' Snake Man' amejinasibu kufanya vizuri pambano hilo kutokana na kupata maandalizi ya kutosha.

'Naomba watanzania wajitokeze kwa wingi kuja kushuhudia pambano hilo ambalo litakuwa na burudani ya aina yake, amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...