Skip to main content

DIWANI LUCY LUGOME KUWAWEZESHA WANAWAKE KWA KUGAWA KUKU BURE


DIWANI wa Kata ya Kisukuru Lucy Lugome, amesema miongoni mwa mikakati yake ndani ya kata ya Kisukuru wilayani Ilala ni kuwawezesha kiuchumi Wanawake kupitia vikundi vyao kwa kugawa kuku bure 50 ili waweze kukuza mitaji yao kupitia vikundi  .

Diwani Lucy Lugome, alisema hayo Dar es Salaam jana, katika mkutano wake wa wananchi ambapo mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo, na mgeni Maalum Meya wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto. 



Wanawake wezangu wa Kusukuru kuna fursa inakuja kwa ajili ya kukuza uchumi kwa kushirikiana na wadau wangu wa Maendeleo hivyo kuna utaratibu maalum utawekwa, utaratibu kupitia vikundi vyenu muweze kupata kuku bure kupitia vikundi vyenu tuwawezeshe kiuchumi "alisema Lugome. 

Diwani Lucy Lugome  aliwataka wanawake wa Kisukuru kufuata utaratibu ili waweze kupata fursa hiyo kila mmoja kwani Kisukuru ya kisasa ya maendeleo inakuja .

Aliwataka wananchi, na wanawake wa Kisukuru kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan za. Utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi na kuleta maendeleo ambapo kisukuru ya sasa imebadirika fursa za uchumi zinapatikana. 


Akizungumzia miundombinu ya Barabara alisema barabara za kisasa zinazojengwa Kisukuru kwa kiwango cha lami,sekta ya afya Serikali ya Dkt.Samia Suluhu Hassan imeshaekeza fedha kwa ajili kujenga hospitali ya kisasa yenye hadhi ya  Rufaa 

Alisema sekta ya afya eneo la hekari tatu kwa ajili ya ulipaji fidia shilingi milioni 353 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali lipo tayari   ambapo zimetengwa shilingi bilioni 5 kwa ajili ya mradi huo. 

Akizungumzia sekta ya Elimu alisema elimu sekondari kukamilika kwa madarasa matano fedha za UVIKO ,matundu ya vyoo,ununuzi wa madawati 590 na Elimu msingi vyumba vitano vya madarasa na uchimbaji kisima cha maji.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...