Skip to main content

HUU HAPA MSIMAMO WA NLD KUELEKEA UCHGUZI MKUU

 

Chama Cha National League for Democracy (NLD) kimesisitiza kuwa hakina mpango wa kushirikiana na chama kingine chochote cha siasa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu 2025.

Akizungumza mapema leo februari 23, 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kamati kuu jijini Dar es salaam katibu mkuu wa chama hicho, Doyo Hassan Doyo amesema historia mbaya walioipata  katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 mara baada ya kushiriki na kuungana na vyama vingine kupitia umoja wa UKAWA chama hakipo tayali kushirikiana na chama chochote kwa sasa.

"Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 chama chetu kilikuwa moja ya vyama vilivyoshiriki kuunda umoja wa UKAWA na kuzunguka kufanya kampeni nchi nzima kwa kutoa mda, asilimali zetu lakini baada ya kutangazwa kwa matokeo chama akikuweza kupata faida yoyote zaidi ya kuwanifaisha wengine kwa kupata wabunge na madiwani nchi nzima". Alisema Doyo

Alisema kufatia madhira hayo na siku za hivi karibuni kumekuwepo na tamko la CHADEMA lililotolewa kupitia Mwenyekiti wake Tundu Lissu "No reforms, no election" NLD haitaunga mkono msimamo huo, nabadala yake itajikita katika kuwatangazia wananchi sera zake ili kupata lidhaa ya kushika nafasi mbalimbali za uongozi.

Doyo aliongeza kuwa Vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu nchini vipo 19, ikiwemo chetu cha NLD, sisi hatuendi kwa msituni wala hatususii uchaguzi, bali tunaenda kuwaeleza wananchi sera za chama chetu ili kupata lidhaa ya kuongoza.

"kelele Zote zinazopigwa kuhusu kushirikiano ni unafiki, chama kitakachokuja kutuambia tujiunge kuiondoa CCM, chama hicho tunakiona ni adui yetu namba moja kwani tulishawahi kushirikiana nao kupitia UKAWA lakini hatukuwahi kunufaika na Muungano huo wa kisiasa". Alisema Doyo na kuongeza kuwa

"Ili Muungano uwe wenye tija kwa vyama vyote ni lazima uweke wazi na pasi na shaka kuhusu namna kila chama kitakavyonufaika baada ya uchaguzi na mgawanyo wa haki wa majimbo kwa vyama vya siasa ili kila chama kinufaike".
Awali akizungumza wakati akifungua mkutano wa kamati kuu ya chama hicho, Mwenyekiti wa chama NLD Taifa, Mfaume Khamis Hassan amewaasa Watanzania kuendelea kudumisha amani ya nchi na kuviepuka vyama vya siasa ambavyo vimekua vikichochea uvunjifu wa amani Nchini.

"Nitoe rai kwa wananchi kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano tulionao nchini hasa kipindi hiki tukielekea katika uchaguzi mkuu kwa kuviepuka vyama vya siasa ambavyo vimekua vikionyesha wazi kuwa na ajenda za kuchochea uvunjifu wa amani Nchini". Alisema Hassan.

Katika hatua nyingine Bw. Hassan ametoa Serikali kuchukua hatua za makusudi kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo kuwapatia ajira ya kudumu walimu wanaojitolea.

Alisema walimu hao wamekuwa wanafanya kazi kubwa hivyo nitoe rai kwa serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan iwangalie kwa jicho la kipekee na kutatua changamoto hiyo kwa kuwapatia ajira za kudumu.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...