Skip to main content

KAMATI YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA UANDAAJI WA MPANGO KAZI WA KITAIFA WAKUTANA DAR



Na Mwandishi wetu 

Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa Uandaaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara imefanya kikao maalum kuhakikisha kuwa rasimu ya mpango kazi huo inakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu ndani ya mazingira ya biashara

 Aidha, pamoja na mambo mengine timu hiyo ya wataalam imekabidhi rasimu ya awali ya mpango kazi huo kwa kamati lengo ikiwa ni kufanya mapitio na kuidhinishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Khamis Hamad amesema kuwa, mpango kazi huo utakuwa na mikakati ambayo inahusiana na masuala ya haki za binadamu katika shuguhuli za kibiashara, Serikali baada ya kuridhia itaikabidhi wizara ya katiba na sheria ya Tanzania bara na Zanzibar kwa ajili ya kuratibu mchakato mzima.

Aidha, kikao hicho kimejumuisha wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia, na wataalam wa masuala ya haki za binadamu na biashara pamoja na makatibu wa kuu wa katiba na sheria kutoka bara na Zanzibar na Wizara ya fedha kutoka pande zote mbili. 

"Na tume ilianza kuratibu mchakato huo kwa kukusanya maoni ya watu wa haki za binadamu na biashara ikiwemo kwenye migodi, sekta ya nishati, tume ikatengeneza  tathimini ya haki za binadamu na biashara kwaajili ya kutengeneza rasmu ya mpango kazi wa haki za binadamu na biashara na kukabidhi kwa kamati ya kitaifa." amesema 

Amesema mpango kazi huo upo kwaajili ya maboresho na kufikishwa serikalini ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa kwa taratibu zaidi mpaka kufikia 2030.  

"Tunaamimi serikali yetu inaonesha dhamira nzuri na nia nzuri katika mpango kazi huo wa kitaifa wa haki za binadamu na biashara kwa rasimu hiyo imefikia sehemu nzuri." amesema

Awali akizungumza wakati wa kikao, amepongeza juhudi za timu ya wataalam katika kuandaa rasimu hiyo na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wadau wote ili kuhakikisha kuwa mpango kazi huo unakuwa nyenzo madhubuti ya kuimarisha uwajibikaji wa makampuni katika kuheshimu haki za binadamu.

Baada ya mapitio ya Rasimu hiyo, wajumbe wa Kamati wamejadili kwa kina vipengele muhimu vya Mpango Kazi huo, huku wakitoa mapendekezo ya maboresho kabla ya hatua za mwisho za kuidhinisha na kuanza utekelezaji wake.

"Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara unalenga kuimarisha mazingira ya biashara nchini kwa kuhakikisha kuwa haki za binadamu zinazingatiwa ipasavyo katika shughuli za kibiashara, kulingana na Miongozo ya Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Haki za Binadamu." amesema Khamis

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...