Skip to main content

RC CHALAMILA KUWAONGOZA WATANZANIA PAMBANO LA KNOCK OUT YA MAMA


IKIWA yamebaki masaa chache kushuhudiwa kwa mapambano kali la ngumi ambalo lilikuwa linasubirowa kwa hamu kubwa, imeelezwa kuwa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert  Chalamila anatarajiwa kuwaongoza Watanzania kushuhudia  mapambano hayo ya ngumi yasiyokuwa ya kuwania mkanda yanayopigwa leo, Feb 28 katika Ukumbi wa Magomeni Sokoni jijini humo.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimepatikana wakati mchakato wa kutambulisha mabondia watakaotwangana leo katika ukumbi huo, kwamba Mkuu wa Mkoa huo, Chalamila atakuwa miongoni mwa viongozi watakaokuwemo ukumbini humo kushuhudia mapambano hayo.

"Wakati tukiendelea 'Face Off' kwa mabondia watakaopigana (kesho), leo nimepata taarifa kuwa Mkuu wetu wa Mkoa anatufuatilia kupitia mitandao ya Kijamii ambayo ipo mubashara kwa sasa na ameahidi kuwepo kushuhudia," alisikika mmoja wa washehereshaji akisema.

Mchakato wa kutambulisha mabondia hao lililokwenda sanjari na tambo kutoka kwa mabondia ilisababisha bondia Abdallah Pazzy 'Dullah Mbabe' almanusura azichape kavukavu na mpinzani wake.

Awali kabla ya mchakato wa show face off kufanyika jioni ya jana Feb 27, 2025 mabondia hao walipata nafasi ya kupima uzito asubuhi huku wadau mbalimbali wakitarajiwa kuhudhuria pambano hilo lenye mvuto wa kipekee.

Pambano hilo linatazamiwa kwa hamu kubwa na kuvuta husia za mashabiki wengi ni kati ya mtoto wa Rashid Matumla Snake Man', Amiri Matumla dhidi ya Mnamibia, Pauls Amavila ambalo litakuwa 'Main Card'

Mkurugenzi wa Mafia Promotion, Ally Zayumba, akizungumza baada ya tukio hilo, amesema kutakuwa na mapambano 14 kwa mabondia wa ndani na nje ya nchi kuoneshana ubabe.

Ameongeza kuwa huo ni msimu wa tatu wanaandaa mapambano hayo 'Knockout ya Mama' lengo kubwa ni kuunga mkono juhudi anazofanya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza michezo na kunadi miradi iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita. 

"Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais Dkt Samia kwa kutubeba katika michezo, wengi mmeshudia kuna goli la Mama, pia amefanya mengi katika sekta ya masumbwi nasi tunandaa mapambano haya ili kuunga mkono juhudi zake," amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...