Skip to main content

SHIGONGO AFUNGUKA MAZITO KUHUSU BUCHOSA, AMPA MAUWA YAKE DKT SAMIA


Mbunge wa Jimbo la Buchosa, wilayani Sengerema Erick Shigongo amesema ana kila sababu ya kumpongeza na kumshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa maendeleo makubwa aliyoyafanya jimboni kwake.

Akizungumza na waandishi wa habri leo jijini Dar es Salaam Mbunge huyo amesema Rais Dkt Samia amefanyia mambo makubwa ikiwemo kugusa sekta zote muhimu ikiwemo afya, elimu, maji ambapo huduma zote hizo hapo awali ilikua ngumu kupatikana kwake.

Amesema kuwa, yeye amekua ni shuhuda namba moja kwa maendeleo hayo kwani alikua akitembea umbali wa kilomita tisa kwenda na kurudi shule ambapo kwa sasa kadhia hiyo imebaki historia.

"Ndani ya miaka minne ya uongozi wa Serikali ya awamu ya sita, mimi kama mbunge wa Jimbo la Buchosa nimepokea zaidi ya bilioni 62.3 ambapo tumejenga barabara, Sekondari mpya 8, Zahanati 21 vituo vya Afya 5, hilo linatosha kusema kwamba Serikali ya Dkt Samia anawapenda wanabuchosa"amesema Shigongo.

Amesema pamoja na kuyumba kwa uchumi wa dunia baada ya janga la ugonjwa wa COVID-19 lakini Tanzania imepambana kurejesha uchumi wake kufikia asilimia 5 ambapo hapo awali ulishuka kutoka asilimia 6 hadi kufikia asilimia 3 na kwa sasa ni moja ya mataifa yenye uchumi mzuri hivyo watanzania wana kila sababu ya kujivunia uchumi wao.

Ameongeza kuwa, Tanzania ni nchi tajiri sana kwa rasilimali ikiwemo gesi asilia, makaa ya mawe,madini ya almasi,tanzanite na madini mengine huku katika sekta ya utalii ikiwa ni nchi ya pili duniani baada ya Brazil huku ikiwa namba 1 kwa Afrika nzima katika sekta ya utalii.

"Nataka niwambie Tanzania ni nchi tajiri sana duniani kwa gesi asilia ni nchi ya 82, makaa ya mawe ni nchi ya 50, Dhahabu ni nchi ya 22, Almasi ni nchi ya 10 na Tanzanite ni nchi ya 1 huku upande wa utalii ikishika nafasi ya pili duniani "

Ameongeza "Hivi karibuni nilizungumza kule New York,Marekani kuwa Afrika ni bara lenye utajiri mkubwa wa rasilimali lakini imeshindwa kubadilisha rasilimali hizo kuwa fedha lakini kwa uongozi bora wa nchi yetu Tanzania,Sasa tunatumia utajiri wetu kujiletea maendeleo na Rais Dkt Samia ameamua kutumia utajiri huo kuanza na sekta ya utalii ambao kwa Sasa unaingiza fedha nyingi na pia anaitumia sekta ya Kilimo katika kukuza kipato"amesema.

Amesema watanzania wanatakiwa kumuunga mkono Rais Dkt Samia kwa kuhakikisha wanashiriki vyema katika kuchangia Pato la Taifa (GDP) kupitia sekta mbalimbali za uchumi ili kuendelea kukuza uchumi Wetu na kuongeza kuwa kama Tanzania itaenda kama ilivyo hivi Sasa basi baada ya miaka 15 itakuwa ni miongoni mwa mataifa tajiri zaidi duniani.

Akizungumzia kuhusu mipaka ya kibiaashara Afrika, Shigongo amesema ni wakati wa bara hilo kuamka na kuwa wamoja huku akilitolea mfano Taifa la Marekani ambalo halina mipaka kwenye majimbo yake kibiashara hivyo ni wakati kwa waafrika kuwa kitu kimoja kwa kukataa kuchonganishwa na nchi za Afrika zifanye biashara zenyewe kwa zenyewe na kuepuka kutumia fedha nyingi kuagiza bidhaa kutoka nje.

''Ukienda Marekani ukapanda ndege kutoka New York kwenda Jimbo lingine huhitaji viza na biashara zinafanyika kwa ushirikiano mkubwa lakini Afrika hatufanyi hivyo kwa hiyo ni wakati wetu Sasa kuamka na kukataa kuchonganishwa"

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...