Skip to main content

CUF YATOA MSIMAMO WAKE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 202

 


Na Mwandishi Wetu, Dar 

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Prof Ibrahim Lipumba amesema kuwa kutokana na mapendekezo kadhaa yaliyotolewa na vyama vya siasa ni vyema uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ungefanyika baada ya marekebisho ya Sheria na Tume Huru ya Uchaguzi pamoja na upatikanaji wa Katiba Mpya.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema kuwa bila ya kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi ni ngumu sana haki kupatikana kwani waliokutana miaka minne imefika hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika, huku akitaka kuwepo na rasimu ya mabadiliko itakayojenga demokrasia .

"Katika kuadhimisha miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi wadau wa siasa tulikutana pale Dodoma mwaka 2021  kila chama kilinaso sera zao huku wakitoa mapendekezo kadhaa ikiwemo kupatikana kwa tume huru, katiba mpya, sheria ya vyama vya siasa ipitiwe upya pamoja na kuwepo kwa michakato shirikishi"

Amesema kuwa, uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na 2024  haukua huru wala haki, bali ulikua unyonyaji wa demokrasia, huku akitoa rai urudiwe, pia amesisitiza Uchaguzi Mkuu ujao ufanyike baada ya marekebisho ya sheria.

Aidha, amesema Chama hicho  hakipo tayari kuungana na vyama vingine vya siasa ili kuing'oa  CCM, wala kuingia kwenye mtego wa mwaka 2015 kwani walipoteza viti vingi na kugeukana wao kwa wao  hivyo hatoshirikiana na chama chochote.

Prof Lipumba amesema uchaguzi wa mwaka 2015 waliamini kuwa wanaunganisha vyama kwa dhati, kumbe chama kingine kipo kimkakati kudhoofisha vingine kutokana na uchu wa madaraka.

"Wakati ule tulipokuwa UKAWA, nikiamini tuko pamoja wakati na narudisha fomu ya kugombea kiongozi mmoja wa chama (jina kapuni) ambaye tulikuwa naye katika muungano huo alikuja kuniwekea pingamizi dakika za mwisho jambo ambalo liliniumiza sana," amesema.

Pia aliongeza kuwa wakati wa ujazaji wa fomu kwa wagombea wa CUF, viongozi wa chama kingine (jina kapuni) waliwashawishi wajaze kama wanatoka kwenye vyama vyao na hiyo inadhihirisha walijipanga kudhoofisha vyama vingine.

Kulingana na changamoto hizo zilizojitokeza wakati huo wa kuunganisha vyama kwa lengo la kuwa na nguvu ya pamoja ili kuking’oa madarakani Chama Cha Mapinduzi (CCM), Prof Lipumba amesema kwa sasa wako ngangali na hawaofii kuunganisha vyama kikubwa wataongeza umakini.

Pia Prof Lipumba amesisitiza kwamba wakati Uchaguzi Mkuu ujao ukiwa umebakisha miezi michache kufanyika ni vizuri uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika mwaka jana ukarudiwa akimiani haukuwa huru na haki.

Wakati Prof Lipumba akitoa misimamo hiyo, pia amewaka wazi kuwa kwa sasa kamati ya chama hicho inayoshughulikia uwandaaji wa Ilani ya Uchaguzi inaendelea na mchakato huo kwa kutumia akili Mnemba (AI) ili kupata mawazo mapana ya kusaidia kufikia malengo stahiki.

"Kamati yetu inaandaa ilani ya uchaguzi kwa kutumia akili Mnemba na imani yetu itatatua changamoto mbalimbali zilizopo na kupata ilani iliyobora, pia watanzania wanatakiwa kufahamu kuwa uchaguzi ni gharama, hivyo watuunge mkono kwa lengo la kuleta mabadiliko,"amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...