Skip to main content

KILWA YAENDELEA KUFURIKA WATALII




Meli ya "Le Bougainville yaleta wengine zaidi ya 130.

Na Beatus Maganja

Meli ya Kifahari ya kitalii ya "Le Bougainville,"  imewasili leo Machi 05, 2025 katika Hifadhi ya urithi wa utamaduni wa dunia Magofu ya Kale Kilwa Kisiwani na Songo Mnara Mkoani Lindi ikiwa na jumla ya watalii 133 kutoka Mataifa mbalimbali duniani Kwa ajili ya shughuli za utalii. Hii ikiwa ni safari  yake ya 7 tangu kuanza kwa msimu wa utalii wa Mwaka 2025

Watalii waliotembelea hifadhi hiyo  wametoka Mataifa ya  Denmark, Australia, Canada, Ufaransa, Marekani, Uingereza na Afrika Kusini huku wengine wakitokea Mataifa ya Uswisi, Romania, Ujerumani, Ubelgiji, New Zealand, na Ireland

Meli hii ya kifahari inahudumia wageni kutoka pande zote za dunia, ikitoa fursa Kwa watalii kutembelea maeneo ya kihistoria na kiutamaduni ya Kilwa, ambayo ni urithi wa dunia wa UNESCO na kuwawezesha watalii  kushuhudia  tamaduni za kiasili zinazopatikana katika hifadhi hii ya kipekee iliyo chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA.

Kwa mujibu wa maafisa wa hifadhi hiyo, safari hii ni sehemu ya juhudi za kuendeleza utalii wa kipekee katika mikoa ya Kusini, huku wakisisitiza umuhimu wa utalii endelevu ambao unaleta faida kwa jamii za maeneo husika. Hii ni meli ya saba kuwasili katika hifadhi hiyo tangu kuanza kwa mwaka huu ambayo mpaka kufikia leo imefikisha jumla ya watalii 854  na inatarajiwa kuongeza idadi ya wageni zaidi katika miezi ijayo.

Wageni wamepata fursa ya kujifunza mengi kuhusu historia ya Kilwa, ikiwa ni pamoja na magofu ya Kilwa Kisiwani  maeneo ambayo yalikuwa ya kibiashara na utawala katika zama za utawala wa Kiarabu na Ureno, pia wamepata fursa ya kushirikiana na jamii za wenyeji.

Meneja wa hifadhi ya Kilwa, Mhifadhi Mwandamizi (Malikale) SC Kelvin Stanislaus Fella amesema  "Tuna furaha kuona meli ya "Le Bougainville" ikirudi tena na tena, na kuleta wageni kutoka mataifa mbali mbali. Hii ni fursa kubwa kwa utalii wetu na ni hatua muhimu katika kutangaza Kilwa kama kivutio cha kimataifa."

Meli ya "Le Bougainville" ni miongoni mwa meli za kifahari zinazotumia njia za baharini kutoa huduma za utalii katika maeneo ya Afrika Mashariki huku safari hizi  zikiratibiwa na Kampuni ya Akorn ambayo huwapeleka watalii katika  maeneo mbalimbali duniani  na inatarajiwa kuleta wageni wengi zaidi katika msimu wa utalii wa 2025.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...