Skip to main content

MRAMBA: BIASHARA YA KUUZIANA UMEME KUINUFAISHA TANZANIA

 


Afafanua kuuuza na kununua umeme ni jambo la kawaida kwa nchi

Asisitiza kununua umeme kwa Mikoa ya Kaskazini kunamanufaa kwa Mikoa husika

Asema kukamilika kwa Mradi wa TAZA kutainufaisha Tanzania na biashara ya umeme

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba ametoa Ufafanuzi zaidi kuhusu hatua ya Serikali kununua Umeme nchini Ethiopitia kupitia Nchini Kenya hadi Namanga Mkoani Arusha  utaimarisha Upatikanaji wa Umeme katika Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambayo kimsingi kwa sasa inatumia umeme unaozalishwa katika Mikoa ya Kusini.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo tarehe 10, Machi 2025 Jijini Dar es Salaam Mha. Mramba amesema ununuzi wa Umeme kutoka nchi Jirani haimaanishi kuwa nchi iko katika changamoto ya upungufu wa umeme kwa kuwa mpaka sasa Tanzania inazalisha umeme wa kutosha ambao ni Takribani Megawati 3796.

Amefafanua kuwa hatua hii ina faida kwa pande zote mbili kwa kuwa njia itakayotumiwa kununua umeme nchini Ethiopia ndio hiyo itakayotumiwa kuuza umeme kwa nchi zenye Uhitaji.

Akifafanunua zaidi amesema kuwa jinsi umeme utakavyokuwa ukinunuliwa, umeme wa Ethiopia utaingizwa kwenye mfumo wa Gridi ya Kenya na kisha Kenya itatoa umeme kuja Tanzania ikifidia umeme ulioingizwa kutoka nchini Ethiopia.

‘’Makubaliano haya yako ya pande mbili kuna wakati sisi tutanunua umeme na kuna wakati tutatumia njia hiyo hiyo kuuza umeme kwa nchi jirani, tunavyoangalia hali ya Kaskazini kwa sasa tunaona sisi tutachukua zaidi kuliko kupeleka lakini kuna wakati na wenyewe wanaweza wakahitaji umeme na tutatumia njia hiyo hiyo kuwapelekea” 

Ameongeza kuwa kununua na kuuziana umeme kwa nchi si jambo geni na Tanzania kwa muda mrefu imekuwa ikinunua umeme nchini Uganda kwa ajili ya Mkoa wa Kagera, nchini Zambia kwa ajili ya Mkoa wa Rukwa na nchini Kenya kwa baadhi ya maeneo ya mkoa wa Tanga hususani ya mpakani.

Aidha, amesema kuwa Tanzania inaendelea na ujenzi wa njia ya Kusafirisha umeme kutoka Tanzania Kwenda Zambia, ambapo kukamilika kwa Mradi huo kutatoa fursa kwa Tanzania kuuza umeme kwa nchi za Kusini mwa Afrika.

Kuhusu Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere ambalo mpaka sasa limefikia asilimia 99.8 kukamilika amesema limekua na mchango mkubwa wa upatikanaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.

“Kule Julius Nyerere sasa hivi tunatumia umeme tunaouhitaji, kama mahitaji yetu sisi ni Megawati 1908 kwenye Gridi ya Taifa hatuwezi kuzalisha zaidi kwa kuwa umeme utakua hauna matumizi”

Pamoja na hayo Mha Mramba ameeleza kuwa Tanzania imejiunga katika masoko ya Pamoja ya kuuziana umeme ya Ukanda wa Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool-EAPP) na Kusini mwa Afrika (Southern African Power Pool-SAPP) ambapo kwa upande wa Kusini mwa Afrika soko lilishaazishwa na linafanya kazi kwa nchi ambazo tayari miundombinu ilishakamilika na kwa sasa Tanzania inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa TAZA ambao kukamilika kwake kutaifanya Tanzania kutumia fursa ya umeme wa unaozalishwa kwenye Bwawa la Julius Nyerere na vyanzo vingine na kuanza kuuza umeme ukanda wa kusini mwa Africa (SAPP).

Hivyo lengo kuu la kuuza au kununua umeme ni kuimarishwa kwa mifumo ya Gridi za Umeme za nchi husika pamoja na kupunguza gharama.Kwa kuzingatia jiografia ya Tanzania itatumia nafasi ya masoko haya ya umeme kununua na kuuza umeme kutoka ukanda wa Mashariki na kusini mwa Afrika.

Serikali kupitia Wizara ya Nishati inaendelea kuhakikisha kunakuwepo na miundombinu imara itakayowezesha manunuzi na mauziano ya umeme ndani ya ukanda wa EAPP pamoja na ukanda wa SAPP ili Tanzania inufaike kwa kuuza na kununua umeme lakini pia kuingiza fedha zitokanazo na gharama za kupitishia umeme kutoka ukanda mmoja kwenda mwingine.

Wakati Miradi mbalimbali ikiendelea kutekelezwa kwa kasi kubwa, kuingiza umeme Ukanda wa Kaskazini kuna faida kubwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha hali ya upatikanaji umeme kwenye mikoa

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...