Skip to main content

TAWA Yasherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa Kutoa Misaada na Elimu ya Uhifadhi



MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA Kanda ya Magharibi leo Machi 3, 2025 imesherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii na uhifadhi, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kulinda wanyamapori na mazingira.

Katika maadhimisho hayo, Kanda hiyo ilitoa misaada ya vyakula kwa wanafunzi wenye uhitaji kutoka Shule ya Wanafunzi wenye changamoto ya uoni ya Furaha ikiwemo mchele, unga, mafuta, sukari na sabuni vyote vikiwa na thamani ya shillingi millioni moja. 

Misaada hii imelenga kuwasaidia wanafunzi hao  na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum.

Vilevile  TAWA ilitembelea Shule ya Sekondari Fundikila na kutoa miche 4000 ya miti ya matunda ya muda mfupi, ikihamasisha upandaji wa miti na kutoa elimu kuhusu uhifadhi wa mazingira. Shule ya Sekondari Kanyenye nayo ilipokea miche 2000 mingine, kama sehemu ya juhudi za kukuza mazingira bora na endelevu kwa jamii.

Akikabidhi misaada hiyo na miche ya miti Kaimu Kamanda wa Uhifadhi wa Kanda ya Magharibi Lupondije Nyanda ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Tabora kushirikiana na Serikali katika jitihada za kulinda rasilimali wanyamapori ikiwa ni pamoja na  kutunza mazingira yao huku akiwahamasisha kutembelea vivutio vya utalii hususani bustani ya wanyamapori hai almaarufu Tabora ZOO.

Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori Duniani Kitaifa yaliyanyika katika viwanja vya ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Dodoma mgeni rasmi akiwa ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...