Skip to main content

FURAHIKA YAWAFIKIA WAFANYAKAZI YAJA NA MPANGO HUU

 




Na Mwandishi wetu 

Wafanyakazi wa Serikali na Sekta binafsi wametakiwa  kuchangamkia fursa ya  kujiunga na Chuo Cha Ufundi  Veta Furahika kwa ajili ya masomo ya jioni kwa kozi mbalimbali 

 Lengo la masomo hayo ya jioni kwa kundi hilo imeelezwa kuwa yanalenga kuwaongezea maarifa yenye tija yatakayoleta ufanisi katika majukumu yao ya kiofisi.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Dkt. David Msuya amesema kwamba masomo hayo yatawasaidia waajiriwa kuongeza ufanisi katika utendaji wa majukumu ya kila siku na kuachana na kufanya kazi kwa mazoea na yataendana mahitaji ya sasa.

"Masomo haya ya jioni kwa waajiriwa wa Serikali na Sekta binafsi yataanza Machi 5, 2025 kuanzia saa 11 jioni hadi 1:00 usiku hivyo tunawakaribisha wote kwa ajili ya ujenzi wa taifa letu," amesema.

Dkt Msuya amezitaja kozi zitakazofundishwa chuoni hapo kwa muda wa jioni kuwa ni Public Administration (Utawala wa Umma), Human Resource Management (HRM), Leadership and  Management pamoja na Project Planning and Management, ambapo kozi zote hizi zitatolewa kwa mwaka mmoja .

Kozi nyengine ni za Fedha na Manunuzi ambapo zinatolewa kwa wiki mbili hadi 12 ambayo ni 'Ethics and Integrity in Public service' itakayotolewa kwa miezi 3, pia itatolewa kozi ya biashara itakayogawanywa katika makundi manne ambayo ni Marketing and Sales, Accounting and Finance, Business administration with Human resources.

Aidha, amesema kuwa chuo hicho, kinatoa fursa sawa kwa watanzania katika kuwaendeleza vipaji vyao na kutoa ujuzi ili waweze kujiajiri badala ya kusubiri ajira za kuajiriwa.

Chuo hicho ambayo kipo Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam kimesajiliwa na NACTVET kwa namba REG/NACTVET/1113 kinatoa kozi mbalimbali ikiwemo hoteli, ushonaji, Ufundi magari, ualimu, ambapo kozi zote hizo hutolewa bure kwa vijana waliomaliza darasa la Saba, kidato cha nne na wale waliokatisha masomo kutokana na changamoto mbalimbali ambazo wamekutana nazo

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...