Skip to main content

SERIKALI INAENDELEA NA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA UMEME – KAPINGA



Lengo ni kuondokana na changamoto ya kukatika kwa umeme

Ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kilindi, Tanga waffikia asilimia 35.

Bilioni 2.63 kulipa fidia wanaopisha njia ya kusafirisha umeme Mkata- Handeni-Kilindi

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya kusambaza umeme ili kuondokana na changamoto ya kukatika kwa umeme nchini.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Aprili 10, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Handeni Mjini, Mhe. Reuben Kwagilwa aliyeuliza ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukatika kwa umeme wilayani Handeni.

"Changamoto ya kukatika umeme Wilayani Handeni inatokana na uchakavu na urefu wa miundombinu ya kusambaza umeme. Katika kukabiliana na changamoto hii Serikali kupitia TANESCO inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya umeme ikiwa ni pamoja na kubadilisha nguzo za miti na kuweka za zege". Amesema Kapinga

Ameeleza kuwa, Serikali kupitia mradi wa gridi imara inaendelea na ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Mkata, Handeni ambacho kipo kwenye hatua za awali za ujenzi.

Ameongeza kuwa, ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kilindi, Tanga umefikia asilimia 35 na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 132 kutoka Mkata kupitia Handeni hadi Kilindi umeffikia asilimia 30.

Akijibu swali la Mbunge wa Mlalo, Mhe. Rashid Shangazi aliyeuliza kuhusu Serikali kuona umuhimu wa kuharakisha ujenzi wa vituo vya umeme vya Mkata, Lushoto na Kilindi kutokana na umuhimu wa vituo hivyo kuimarisha upatikanaji wa umeme Mkoa wa Tanga, Mhe. Kapinga amesema tayari Wizara ya fedha imeihakikishia Wizara ya Nishati kuwalipa wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo kwa wakati ili waikamilishe.

Na kuhusu kusuasua kwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mkata hadi Kilindi kutokana na ulipwaji wa fidia, Mhe. Kapinga amesema fidia ya wananchi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mkata, handeni hadi Kilindi ni takribani shilingi bilioni 2.63 ambayo Wizara ya fedha wameihakikishia Wizara ya Nishati kuilipa fidia hiyo.

Mhe. Kapinga ameongeza kuwa, fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Mkata, Handeni tayari wameshalipwa fidia.

Akijibu swali la Mbunge wa Hanang’, Mhe. Mhandisi Samwel Xaday aliyeuliza ni lini Serikali itatatua changamoto ya kukatika kwa umeme Wilaya ya Hanang’, Mhe. Kapinga amesema Wilaya ya Hanang’ ipo katika mradi wa ujenzi wa gridi imara awamu ya pili ambapo kitajengwa kituo cha kupokea na kupoza umeme ambapo kwa sasa Serikali inaendelea na awamu ya kwanza ya mradi wa gridi imara.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Mhe. Grace Tendega kuhusu kukatika kwa umeme mkoani humo hasa Jimbo la Kalenga, Mhe. Kapinga amesema Serikali inayo mikakati ya kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Iringa ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya umeme kwa kubadilisha nguzo na nyaya chakavu.

Aidha, Mhe. Kapinga amesisitiza kuwa kutokea Mkoa wa Iringa, Tunduma hadi Katavi Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa kusafilisha umeme wa TAZA ambao unahusisha ujenzi wa vituo vya kupoza umeme ambavyo vitaboresha upatikanaji wa umeme maeneo yote ya ukanda huo na kuongeza kuwa mradi huo utaunganisha gridi za Taanzania na Zambia.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...