Skip to main content

STEVE NYERERE KUNOGESHA TAMASHA LA MTOKO WA PASAKA





Na Mwandishi wetu, Dar 

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao Steve Mengele maarufu kama (Steve Nyerere) ni miongoni mwa watu mashuhuri watakaohudhuria katika tamasha la mtoko wa Pasaka litakalofanyika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Steve Nyerere amesema kuwa siku ya sikuu ya Pasaka kutafanyika tamasha kubwa la mtoko wa Pasaka ambapo litawakutanisha wasanii nguli wa mziki wa injili.

"Maombi yana nguvu kuliko mtutu wa bunduki,maombi yana nguvu kuliko matusi,maombi yana  nguvu kuliko kitu kingine chochote,hivyo siku hiyo tutaliombea Taifa na Rais Wetu Mpendwa Dkt Samia Suluhu Hassan "amesema

Ameongeza "sisi tumeona ndani ya mwezi huu(April)kulikua na mambo mengi ikiwemo ramadhani, kwaresma,na sasa tunelekea kwenye sikukuu ya Pasaka,hivyo kuelekea kilele cha sikukuu ya pasaka tutatoa pakeji ya vifaa vya kumsaidia mama mjamzito kujifungua katika Hospitali zote za Wilaya Mkoani Dar es salaam" 

Aidha, Steve amempongeza muimbaji  mkongwe wa nyimbo za injili Christina Shusho kwa kuandaa tamasha la mtoko wa pasaka litakalofanyika siku ya pasaka April,20,2025 katika ukumbi wa Superdome Masaki kuanzia saa saba mchana.

"Watakuwepo waimbaji wote nguli wa nyimbo za injili kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania Kenya,Uganda na kwingineko,ambapo  watashiriki katika tamasha hilo ambalo halitakua na kiingilio lenye kauli mbiu isemayo "kwa maombi utashinda"

Kwa upande wake Mwimbaji wa Nyimbo za injili Christina Shusho,amesema kwamba tamasha la "mtoko wa pasaka" linafanyika kwa mara ya tatu ambapo limelenga kuwaleta watanzania pamoja na raia wa mataifa mengine ili kufurahi kwa pamoja kupitia nyimbo na muziki wa injili. 

"Siku hii ni Maalum sana kwa ajili ya watu wote , hatuangalii dini wala kabila cha muhimu ni kuvaa na kupendeza, yaani  ukialikwa alikika"amesema Shusho.

Aidha, amesema waimbaji wengi watakutana na kufurahi lakini kwa sababu ni mwaka wa uchaguzi pia watamuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi anazozifanya za kuliongoza Taifa la Tanzania ashinde katika uchaguzi.

Amesema kuwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao imekua ikifanya mambo mengi ya kijamii,hivyo yeye kama mwanachama wa Taasisi hiyo ameamua kuandaa tamasha la nyimbo za injili siku ya sikukuu ya pasaka April 20,2025 ili kufurahi pamoja na jamii.

"Tumealika na watu mbalimbali ikiwemo ndani na nje ya nchi Kwa lengo la kujionea amani na utulivy uliopo nchini humo, huku wakifurahia burudani ya kutosha kutoka kwa wasanii nguli wa mziki wa injili".

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...