Skip to main content

MAPATO YA KIKODI CHANZO CHA MAENDELEO - DKT MPANGO






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema maendeleo ya Tanzania katika uendelezaji miundombinu ni kutokana na ufanisi katika mapato ya kikodi,  ushiriki wa sekta binafsi pamoja na uimarishaji wa masoko ya mitaji na dhamana inayotumika katika kufadhili miradi hiyo.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati aliposhiriki majadiliano ya Viongozi wa Juu kuhusu “Umuhimu wa kutumia Rasilimali za Bara la Afrika kwa ufanisi ili kuchochea Maendeleo” yaliyofanyika wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) unaofanyika katika Hoteli ya Sofitel Ivoire Jijini Abidjan nchini Ivory Coast.

Amesema kutokana na umuhimu wa miundombinu katika mageuzi ya kiuchumi nchini Tanzania, Serikali ilihitaji kufanya kazi zaidi katika kukusanya fedha ya uendelezaji wa miundombinu ikiwemo Reli ya kisasa (SGR) pamoja na barabara kuu ambazo zitaunganisha mataifa mbalimbali na kuwezesha ufanyaji biashara.

Makamu wa Rais ametaja juhudi za serikali katika ukusanyaji mapato ya ndani na kufadhili miradi ikiwemo kuimarisha usimamizi wa kodi kama vile ukusanyaji kupitia mifumo ya kielektoniki, kuwepo kwa Ofisi ya Msuluhishi wa Malalamiko ya walipa kodi ili kuwawezesha walipa kodi kuweza kutoa changamoto zao pamoja na kukuza wigo wa soko la mitaji na dhamana kama vile uwepo wa hatifungani mbalimbali.

Hatua zingine ambazo Tanzania imepitia katika kuimarisha miundombinu ni pamoja na matumizi ya mifuko ya hifadhi ya jamii katika ujenzi wa barabara na madaraja pamoja na kutumia vema mikopo nafuu kutoka mashirika ya fedha kimataifa na nchi marafiki.

Makamu wa Rais ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na Rais wa AfDB anayemaliza muda wake Dkt. Akinumwi Adesina kwa kushirikiana vema na Tanzania katika kipindi cha uongozi wake ikiwemo kuwezesha ujenzi wa barabara, uwanja wa ndege pamoja na reli ya kisasa (SGR) kuelekea nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo.

Makamu wa Rais amesema Tanzania imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya nishati kwa lengo la kuharakisha maendeleo ikiwemo uwekezaji mkubwa katika mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ambao umekamilika na unazalisha megawati 2115. Pia uwekezaji katika miradi mingine ikiwemo matumizi ya gesi asilia pamoja kuanza uzalishaji wa nishati ya joto ardhi ambayo itaanza kwa kuzalisha megawati 500.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...