Skip to main content

REDET, PPPC KUFANYA KONGAMANO

 




Na Mwandishi wetu Dar 

Kituo cha Ubia kati Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa masuala Demokrasia (REDET) chini ya Chuo Kikuu Cha Dar es salaam  wameandaa kongamano kwa ajili ya kujadili nafasi ya sekta binafsi na sekta ya umma kuelekea dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 .

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo,  Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia (PPPC) David Kafulila, amesema moja ya majukumu ya PPPC ni kuiwezesha jamii kupata uelewa  juu ya masuala ya kisera na kisheria na mipango ya Serikali katika maeneo ya ubia 

Aidha, amesema kongamano hilo ambalo litakuwa la wazi linatarajia kufanyika Mei 27,2025 katika ukumbi wa Maktaba katika Chuo Kikuu Cha Dar es salaam ambapo limelenga kuwashirikisha wadau mbalimbali ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa.

"PPPC iliona ipo  haja ya kushirikiana na Taasisi ya REDET ambayo imebobea katika uendeshaji wa makongamano kwa lengo la  kuushirikisha umma zaidi,

Taasisi ya REDET imekuwa ikifanya vizuri katika shughuli za makongamano na midahalo katika miongo mingi zaidi"amesema Kafulila 

Aidha amewaomba watanzania kushiriki katika kongamano hilo ambalo ni la wazi kwa ajili ya kutoa maoni na kusikiliza ili waweze kujifunza zaidi katika kufikia maendeleo ya dira ya Tanzania 2025.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya REDET, Profesa Rwekaza  Mukandala amesema kongamano hilo litakuwa na mada ndogo zitakazowasilishwa.

Akitaja mada hizo ni pamoja Dola, Masoko na Uhamasishaji wa Mitaji nafasi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Aidha amesema kongamano hilo litaudhuriwa na Maafisa waandamizi wa Serikali, wakuu wa makampuni ya sekta binafsi, wanazuoni na wawakilishi wa kada nyingine mbalimbali.

Profesa Mukandala amewaomba wananchi kuhudhuria kongamano hilo la wazi ili waweze kushiriki kwenye mjadala kuhusu dhana ya PPP Center na nafasi yake kwenye kutekeleza Dira ya Taifa 2050.

Amesema katika mada hizo Mkurugenzi wa PPPC, David Kafulila atafanya wasilisho kuhusu dhana ya PPP Center na nafasi yake kuelekea Dira ya Taifa 2050 na Mwenyekiti wa REDET, Profesa Rwekaza Mukandala, ataongoza kongamano hilo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...