Skip to main content

WAKILI MADELEKA AJITOSA JIMBO LA KIVULE




Wakili Peter Madeleka leo amechukua fomu ya kugombea Ubunge  Jimbo la Kivule kupitia tiketi ya Chama cha Act Wazalendo .

Mapema leo amefika katika katika Ofisi za Chama cha Act Wazalendo zilizopo Jimbo la Kivule Kata ya Kitunda, akiwa na wafuasi wa Chama hicho kuchukua fomu hiyo na kuomba ridhaa ya Chama hicho kumpitisha kugombea Jimbo hilo. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mara baada ya kuchukua fomu hiyo amesema ameamua kugombea Jimbo hilo ili kuweza kuwasaidia wananchi kutokana na changamoto nyingi za kijamii zinazowakabili Jimbo humo.

"Jimbo hili ni jipya lakini hakuna maendeleo yoyote yaliyoletwa, barabara ni mbovu hazipitiki mvua zikinyesha mawasiliano yanakua shida, limesahaulika kwa muda mrefu sasa nimekuja mkombozi wao"amesema Wakili Madeleka

Amesema kuwa, miongoni mwa ajenda zake atazokwenda nazo endapo chama kitampaa ridhaa ya kugombea katika Jimbo hilo ni kusimamia haki na kuhakikisha anaweka misingi mizuri ya watu kuishi bila maumivu.

"Kila mtu ana haki ya kuishi hakutokua na matekaji wala mauwaji leo ni siku ya kuchukua fomu wakati wa kampeni bado tutaanda siku maalum ya kukaa pamoja kama wanakivule tukajadili matatizo yetu ili mwisho wa siku tuwe na maamuzi ya pamoja ya kuikataa CCM na mawakala wake wote " amesema Wakili Peter Madeleka.

Ameongeza kuwa, Jimbo la Kivule ni miongoni mwa majimbo yanayoongoza kwa shida nchini Tanzania,hivyo kipaumbe chake cha kwanza ni kuhakikisha anaziondoa changamoto za kijamii kama barabara, maji,elimu bora Afya pamoja na kuwapatia umeme wa uhakika.

Amesema kuwa, licha ya kuwepo na changamoto nyingi kwenye uchaguzi lakini wao hawawezi kususia uchaguzi kwani wizi wa kura umekuepo muda mrefu lakini watapambana nao wakiwa pamoja, watahakikisha wanalinda kura zao ikibidi hata kulala kwenye vituo vya kumpigia kura.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...