Skip to main content

KATIBU MKUU NILD AHUDHURIA UZINDUZI WA RATIBA YA UCHAGUZI MKUU OCTOBER


Katibu Mkuu wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, ameungana na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa nchini kushiriki hafla ya uzinduzi wa Ratiba ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Madiwani kwa upande wa Tanzania Bara, kwa mwaka 2025.

Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 26, 2025, katika ofisi za Makao Makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), jijini Dodoma, na umeongozwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Jacobs Mwambegele.

Tukio hili limeelezwa na viongozi mbalimbali kuwa ni hatua muhimu katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao, na linaakisi dhamira ya Tume ya Uchaguzi kuhakikisha maandalizi ya uchaguzi yanatekelezwa kwa uwazi, ushirikishwaji na kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi.

Akizungumza baada ya hafla hiyo, Katibu Mkuu wa NLD, Mhe. Doyo, alieleza kuwa chama chake kipo tayari kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Oktober mwaka huu. Alisema kuwa chama kimejipanga kusimamisha wagombea wa udiwani na ubunge katika majimbo na kata zote nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha sauti za Watanzania kutoka kila pembe ya nchi zinasikika kupitia chama cha National League for Democracy.

“Kwa sasa tumeshakamilisha asilimia 85 ya zoezi la ndani la uteuzi na uhakiki wa wagombea wetu, na matarajio yetu ni kuhakikisha tunafikia asilimia 100 kabla ya muda wa uteuzi rasmi kuanza,” alisema Mhe. Doyo. Aidha, aliongeza kuwa chama chake kinasimamia misingi ya uzalendo, haki, maendeleo na usawa jumuishi, na kimejipanga kutoa sera mbadala zinazolenga kuinua maisha ya wananchi wa Tanzania.

Chama cha NLD kimeahidi kuendesha kampeni safi, ya kistaarabu na inayojikita katika hoja na sera, huku kikitoa wito kwa wadau wote wa uchaguzi kuheshimu sheria, taratibu, na misingi ya demokrasia.

Taarifa,

Imetolewa na

Idara ya Mawasiliano

National League for Democracy (NLD)

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...