Skip to main content

KIGOGO MWENGINE CHADEMA ATIMKIA CHAUMMA

 




Na Mwandishi wetu

Aliyekua Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA)Taifa, Sigrada Mligo, ametangaza kujiondoa rasmi ndani ya Chama hicho na kujiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kwa madai kuwa amechoshwa na kauli mbaya zinazotolewa dhidi yake.

Uamuzi huo ameutoa  ikiwa ni miezi kadhaa baada ya kuripotiwa kujeruhiwa na mmoja wa walinzi wa Chadema wakati wa kikao cha ndani kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho John Heche March 25, 2025, mjini Njombe.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es Salaam katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha Chaumma Kinondoni amesema baadhi ya wanachama na viongozi wa Chama cha Chadema wamekuwa wakimtolea maneno na kumdhihaki kwa kumuita msaliti wa Chama licha ya kujitoa maisha yake yote.

Mligo amesema kuwa ameumizwa na namna anavyotajwa kuwa chanzo cha migogoro, licha ya kuwa mmoja wa waliokibeba chama wakati wa kipindi kigumu, hivyo ametumia busara ya kuhama Chama cha Chadema.

"Mwaka 2019 tuliendesha Chadema  Digital ambayo ilikuwa inasajili wanachama na kushughulikia masuala ya uchaguzi, lakini kwenye uchaguzi wa Januari 2025, Chadema ilishindwa kufanya operesheni kwenye majimbo ya Makete, Wang’ing’ombe na Ludewa kwa sababu ya ukosefu wa bajeti. Mimi ndiye nilimpigia Katibu Mkuu Mnyika kuuliza sababu, na yeye akathibitisha kuwa hawana fedha" amesema Mligo.

Mlingo amebainisha kuwa, aliamua kufadhili operesheni hiyo kwa fedha zake binafsi, akitumia zaidi ya shilingi milioni 15 kuhakikisha kuwa majimbo hayo matatu katika Mkoa wa Njombe yanashiriki mchakato wa uchaguzi wa ndani ya chama.

Ameongeza "Niliigharamia kwa fedha zangu hadi majimbo yanapata uongozi ambao ulipiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa chama, zipo kwenye kumbukumbu rasmi, hawawezi kubisha," amesisitiza.

Hata hivyo, Sigrada amesema licha ya kujitolea kwake kwa hali na mali, amekuwa akidhihakiwa na baadhi ya wanachama na viongozi wa Chadema ambao, kwa maneno yake, wanajifanya kuwa wao ndio waliokifia chama kuliko wengine.

"Sasa unakutana na lugha za kienyeji sana ambazo zinataka kuonesha kwamba kuna watu wameipambania Chadema, wameifia kuliko watu wengine, sisi wengine sio watu wa matangazo wala mitandaoni, nikisema niliyoyafanya kwenye chama hiki halafu mtu anakuja na lugha laini kwamba Sigrada anakiua chama, unamshangaa" ameeleza Sigrada.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...