Skip to main content

RAIS SAMIA KUZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA NA UANZAJI RASMI WA TRENI YA MIZIGO YA SGR


Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb), amesema kuwa hafla ya uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala na kuanza rasmi kwa safari za treni ya mizigo ya reli ya kisasa (SGR) kati ya Dar es Salaam na Dodoma itafanyika Julai 31, 2025, Kwala, mkoani Pwani, ikihusisha pia upokeaji wa mabehewa mapya na yaliyokarabatiwa ya reli ya zamani (MGR) ambapo Mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na Wanahabari kwenye ukumbi wa TPA Jijini Dar es salaam leo tarehe 25 Julai,2025 Waziri Mbarawa amesema Bandari Kavu ya Kwala, iliyojengwa Vigwaza, kilomita 90 kutoka Dar es Salaam, ina uwezo wa kuhudumia makasha 823 kwa siku (takribani 339,500 kwa mwaka), sawa na asilimia 30 ya makasha yote ya Bandari ya Dar es salaam na kueleza kuwa eneo hilo lilichaguliwa kutokana na jiografia nzuri na ardhi ya serikali isiyo na migogoro.

Ameongeza kuwa, treni ya mizigo ya SGR imeanza rasmi kutoa huduma kuanzia tarehe 27 Juni, 2025 baada ya majaribio kufanyika, ambapo imepunguza muda wa kusafirisha Mizigo  kutoka masaa 16 hadi masaa 4 kati ya Dar es Salaam na Dodoma na tayari makampuni kama Azania Group na Dangote Cement zimeshanufaika na huduma hiyo.

Amesema Serikali ya awamu ya sita inaendelea kuboresha reli ya zamani (MGR) kwa kupokea mabehewa 50 mapya na 20 yaliyokarabatiwa ili kuongeza uwezo wa kusafirisha mizigo nchini na kukuza uchumi.

Faida zitakazopatikana ni pamoja na Kupunguza msongamano bandarini na barabarani, Kuongeza ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam, Kupunguza ajali gharama za usafirisaji sambamba na kukuza ajira na biashara katika Mikoa jirani

Waziri ametoa mwito kwa wananchi na wadau wa usafirishaji kuhudhuria hafla hiyo na kuchangamkia fursa za kiuchumi zinazotokana na miradi hiyo muhimu kwa maslah ya Taifa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TPA Bw.Plasduce Mbosa amesema Mamlaka imejipanga kikamilifu kuhakikisha bandari ya Kwala inatoa huduma bora na za kiwango cha kimataifa 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TRC Mha Machibya Shiwa amesema TRC itaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha huduma ya usafiri wa reli inaimarika nchini.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...