Skip to main content

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA, WAPEWA SOMO NA JAJI MUTUNGI

 


Na Mwandishi wetu

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama vya siasa nchini kujiepusha na lugha za matusi, kashfa, uchochezi au vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga amani na utulivu wa taifa la Tanzania hasa kuelekea uchaguzi Mkuu.

Wito huo ameutoa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa ambapo amesisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuendeleza misingi ya amani na mshikamano wa taifa.


Amesema kuwa, viongozi wa vyama vya siasa nchini ni vyema kuhakikisha kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 zinafanyika kwa kistaarabu, bila kutumia lugha za matusi, kashfa au vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha tunu ya amani Taifa iliyopo.

"Nendeni mkafanye kampeni za kistaarabu mkiwanadi wagombea wenu, kuweni na lugha nzuri za kuzungumza, epukeni matusi, lugha za kashfa, kwani amani ya taifa hili ni muhimu kuliko chochote"mesema Jaji Mutungi.

Ameongeza kuwa, amani na mshikamano ni urithi ulioachwa na waasisi wa taifa, hivyo viongozi wa kisiasa wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa wananchi.


"Kumbukeni kuna maisha baada ya uchaguzi, Uchaguzi si mwisho wa siasa wala maendeleo. Turithishe amani hii kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo," amesema Jaji Mitungi.

Sambamba na hayo amewasihi , viongozi kutokubabaishwa na upotoshaji unaoweza kusambazwa kupitia mitandao ya kijamii na makundi mengine katika jamii akisisitiza kuwa uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa taarifa zinazoleta taharuki wawe nazo makini.


"Mtaambiwa uchaguzi haupo, msikate tamaa. Uchaguzi upo, na jambo kubwa zaidi ni kuhakikisha tunaingia kwenye uchaguzi huru na wa haki kwani ninyi ndio wakala wa kwanza wa kuhakikisha hilo linatekelezeka," amehimiza.

Kwa upande wake,  Mwasilishaji Kuhusu Sheria Wakili Edmumdi Mgasha amebainisha kuwa Kifungu cha kanuni za Uchaguzi 6(,1)(2) kinamtaka Msajili kuweka pingamizi dhidi ya Mgombea aliyeshindwa kuweka Wazi kiasi cha vyanzo vya gharama za Uchaguzi ndani ya siku 14 baada ya uteuzi.


Naye, Mwenyekiti wa Baraza la vyama vya Siasa Juma Khatib amewataka viongozi na watendaji wa vyama vya Siasa kuzingatia kwa makini masharti ya sheria ya gharama za uchaguzi ili kuepusha dosari na kasoro katika uchaguzi mkuu wa Octoba 2025.

Amesema kuwa, historia inaonesha baadhi ya vyama vya Siasa na wagombea walikua na uwelewa mdogo walipotakiwa kuwasilishwa taarifa za gharama za uchaguzi jambo ambalo limesababisha dosari kubwa ndani ya uchaguzi.


"Sheria hii ilipokuja mwaka 2010 watu wengi hawakuwa na uwelewa wengine walijaza gharama za uchaguzi hewa wakidhani baada ya uchaguzi wanarejeshewa fedha baada ya uchaguzi, walitengeneza risiti za kughushi, kumbe haipo hivyo, leo tutapata elimu ya kutosha"amesema Khatib.

Aidha, amewataka viongozi hao kuyachukua mafunzo hayo kwa umakini mkubwa sana ili kuepusha migogoro hasa kuelekea kipindi hiki Cha uchaguzi, zoezi hili liendeshwe kwa uwazi na uadilifu.









Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...