Skip to main content

WALIMBWENDE WA MISS GRAND TANZANIA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HIFADHI YA PANDE




Na Beatus Maganja,

Dar es Salaam

Walimbwende 24 wanaoshiriki mashindano ya Miss Grand Tanzania 2025 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara, wamefanya ziara ya siku moja katika Hifadhi ya Pande iliyopo jijini Dar es Salaam tarehe 13 Agosti 2025 kwa lengo la kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii wa ndani.

Ziara hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano kati ya waandaaji wa Miss Grand Tanzania na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha walimbwende hao kujifunza masuala ya uhifadhi na utalii na kuwa mabalozi wa vivutio vya utalii wa ndani, hususan Hifadhi ya Pande.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Kamanda wa Hifadhi ya Pande, PC Suleiman Keraryo, alisema hifadhi hiyo ni kivutio cha kipekee kilichopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo wageni hupata fursa ya kutalii na kujionea vivutio mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kujifunza kuhusu historia ya hifadhi hiyo, bioanuwai na mchango wake katika uhifadhi wa mazingira na viumbe hai.

“Karibuni sana katika Hifadhi yetu ya Pande, hifadhi iliyo katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ikiwa na wanyamapori wa aina mbalimbali na vivutio vingine lukuki. Hapa ni mahali sahihi kwenu kujifunza na kujionea rasilimali za nchi yenu,” alisema Keraryo.

Aidha, alibainisha kuwa mshindi wa Miss Grand Tanzania 2025 atateuliwa kuwa Balozi wa Hifadhi ya Pande, ambapo atashirikiana na TAWA katika juhudi za kuitangaza hifadhi hiyo pamoja na kuchochea utalii wa ndani, sambamba na kuunga mkono juhudi za Serikali katika sekta ya maliasili na utalii.

Mashindano ya fainali ya Miss Grand Tanzania yanatarajiwa kufanyika tarehe 16 Agosti 2025 katika Ukumbi wa Superdome, Masaki – Dar es Salaam.

Uongozi wa Hifadhi ya Pande pia umeeleza dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano na waandaaji wa Miss Grand Tanzania kwa kuhakikisha kuwa walimbwende wanapata fursa ya kulala ndani ya hifadhi hiyo na kufanya mazoezi katika mazingira ya asili, ili kuongeza uelewa wao kuhusu uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wao, walimbwende wameeleza kufurahishwa na ziara hiyo, hususan kupata fursa ya kuona kwa ukaribu aina mbalimbali za wanyamapori waliopo hifadhini humo, sambamba na mapokezi mazuri kutoka kwa maofisa wa TAWA. Pia waliahidi kuwa mabalozi wa kuitangaza hifadhi hiyo kwa jamii.

Ziara hiyo imeelezwa kuwa ni mwanzo wa ushirikiano endelevu kati ya TAWA na taasisi za kijamii, hususan zinazowalenga vijana, kwa lengo la kuongeza uelewa juu ya umuhimu wa kulinda mazingira na kuendeleza utalii wa ndani kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...