Skip to main content

DOYO: AHIDI KUSITISHA MIKATABA YA MADINI YENYE HARUFU YA UFISADI


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiwa mkoani Mara, wilaya ya Tarime, amewahakikishia wananchi kuwa endapo atachaguliwa kuwa Rais, atasitisha mikataba yote ya madini na kuipitia upya.

Mhe. Doyo amesema kuwa iwapo itabainika mikataba hiyo imeingiwa kwa njia ya rushwa au ufisadi, serikali yake itaiondoa na kuanzisha mikataba mipya yenye kuzingatia maslahi ya taifa. Aidha, ameongeza kuwa wananchi wazawa wa Tarime watapewa kipaumbele cha kwanza katika uwekezaji wa madini ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania wenyewe.

Akiwa Nyamongo, mkoa wa mara Mhe. Doyo alisisitiza kuwa haiwezekani eneo lenye mgodi mkubwa kama huo likakosa huduma bora za kijamii huku wageni wakiendelea kumiliki utajiri wa taifa. Alitolea mfano wa Saudi Arabia, akieleza jinsi wananchi wa nchi hiyo wanavyonufaika na huduma bora kutokana na mapato ya mafuta, na akasema wananchi wa Nyamongo hawapaswi kubaki wakitegemea kuendesha bodaboda pekee.

Kwa mujibu wa ahadi yake, endapo atachaguliwa kuwa Rais, serikali yake itahakikisha wananchi wa Mkoa wa Mara wanamilikishwa mgodi huo na kunufaika moja kwa moja na mapato yake.

Aidha, Mhe. Doyo amewaahidi wananchi wa Tarime kujengewa soko la kisasa. “Haiwezekani kwa namna Mkoa wenu wa Mara ulivyo na rasilimali nyingi, ikiwemo madini, wilaya ya Tarime ikakosa kuwa na soko la kisasa. Nitahakikisha tunajenga soko lenye hadhi na linalokidhi mahitaji ya wananchi,” amesema.

Mbali na hilo, Mhe. Doyo pia amesisitiza dhamira yake ya kuwekeza katika huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na miundombinu ya barabara, akieleza kuwa maendeleo ya wananchi ndiyo msingi wa ustawi wa taifa.

Kwa sasa, msafara wa mgombea huyo wa NLD upo Kanda ya Ziwa ukiendelea na mikutano yake ya kampeni, ambapo amekuwa akiwahimiza wananchi kuchagua uongozi unaojali maslahi ya wananchi na kulinda rasilimali za taifa kupitia Chama cha NLD.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...