Skip to main content

DOYO KUONDOA SHERIA KANDAMIZI YA KIKOKOTOO





Handeni, Tanga

Mgombea Urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, amehutubia mamia ya wananchi katika viwanja vya Soko la Zamani, Handeni Mjini.

Katika hotuba yake, Mhe. Doyo aliwataka wananchi wa Handeni kutafakari kwa kina changamoto mbalimbali zinazowakabili, ikiwemo tatizo la maji ambalo limekuwa sugu kwa muda mrefu. Mhe. Doyo alisema:

"Tatizo la maji Handeni limekuwepo tangu nikiwa mdogo hadi leo. Chanzo cha maji kiko umbali wa kilometa 50 kutoka Mswaha, lakini maji hayo yamekuwa yakipita hapa Handeni na kuelekea Pangani, kwa sababu tu Waziri wa Maji anatokea Pangani. Hili si jambo la bahati mbaya. Wanahandeni wanapaswa waamke na kuelewa kuwa baadhi ya viongozi siku zote hubeba maslahi yao binafsi. Ukosefu wa maji Handeni si kwa bahati mbaya, bali ni kwa sababu ya kukosa utashi wa kisiasa. Nawaomba mnichague ili twende tukatatue changamoto hii. Wananchi wa Handeni wanahitaji maji kwa haraka na si ahadi tena."

Aidha, Mhe. Doyo aliwahakikishia wananchi kuwa iwapo watampa ridhaa ya kuongoza taifa, atahakikisha wastaafu wote wanapata heshima na haki zao bila kunyanyaswa na sheria zisizo na tija.

"Sheria ya kikokotoo ni kandamizi na inawaumiza watumishi wa umma waliolitumikia taifa hili. Ni dhambi kubwa kwa serikali kuingia mgogoro na wastaafu ambao wametumikia nchi kwa uadilifu. Wastaafu wote wanapaswa kulipwa kwa heshima, na fedha zao kurudi mikononi mwao bila kuchelewa. Nikipewa dhamana ya kuongoza, ndani ya siku 10 baada ya kuapishwa, nitafuta kabisa sheria hii kandamizi. Kila mstaafu atachukua pesa yake kwa uhuru, kwa kuwa hiyo ni amana yake aliyoitumikia katika taifa hili." alisema Mhe. Doyo.

Mikutano ya Mhe. Doyo inaendelea kuvutia mamia ya wananchi kutokana na sera zake zenye maono ya uzalendo, haki, na maendeleo. Msafara wake sasa unatarajiwa kuendelea Manyara na Arusha, huku wananchi wakimsubiri kwa shauku.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...