Skip to main content

DOYO, NITAFUNGUA MASOKO UA NJE KWA WAKULIMA WA LUSHOTO



Na Mwandishi Wetu

Lushoto, Tanga

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NLD, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mhe. Hassan Doyo, ameendelea na kampeni zake kwa kunadi sera za chama katika eneo la Lukozi, wilayani Lushoto.

Katika mkutano huo uliovuta idadi kubwa ya wafanyabiashara wa mboga mboga, Mhe. Doyo alibainisha changamoto kubwa inayowakabili wafanyabiashara hao kuwa ni ukosefu wa masoko ya uhakika. Alieleza kuwa iwapo biashara hiyo itaandaliwa kwa ubora na ustadi, inaweza kuwanufaisha wananchi na familia zao kiuchumi.

“Mazao haya ya mbogamboga yana soko kubwa hata nje ya nchi, lakini tatizo ni kwamba hatujaandaliwa mazingira mazuri ya kibiashara. Kwa sasa mazao yote yanategemea soko moja la Dar es Salaam, na huko nako madalali huwanyonya wakulima. Mkinipa ridhaa, nitahakikisha tunawatafutia masoko ya nje ya nchi. Tutawaleta wanunuzi wakubwa, watasindika mazao yenu na kusafirisha kimataifa. Jiografia ya Lushoto inaruhusu biashara ya mazao haya kufanyika kwa misimu yote,” alisema Mhe. Doyo.

Akizungumza zaidi, Mhe. Doyo aliikosoa serikali iliyopo madarakani kwa kushindwa kuwa wabunifu katika kuwaendeleza wananchi kiuchumi. Alifafanua kuwa sura ya nne ya Ilani ya Chama cha NLD imebeba ajenda ya kilimo, mifugo, uvuvi na usalama wa chakula, akibainisha kuwa takribani asilimia 70 ya Watanzania hutegemea kilimo kama chanzo kikuu cha kipato.

“Tatizo kubwa ni kuwa kilimo chetu kimeendelea kuwa cha mvua na hakina tija. Hata hivyo, ninyi watu wa Lushoto mnabebwa na jiografia ya eneo hili. Changamoto iliyopo ni upungufu wa miundombinu ya kuhifadhi na kusindika mazao,” alisisitiza.

Aidha, aliwahimiza wananchi wa Lushoto kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu na kumpigia kura yeye, Doyo Hassan Doyo, kwa tiketi ya Chama cha NLD, ili kutimiza adhima ya kubadilisha maisha ya wananchi wa Lushoto na Watanzania kwa ujumla.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...