Skip to main content

MTAMBO WA GESI ASILIA WASAFIRISHWA KWENDA MTWARA KUONGEZA NGUVU YA UZALISHAJI WA UMEME

 



Na Agnes Njaala, Dar es Salaam

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika katika mikoa ya Mtwara na Lindi, ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya matumizi ya umeme kutokana na ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii. 

Hayo yanathibitishwa na hatua zilizochukuliwa na Shirika hilo Kusafirisha mtambo  wa Kuzalisha Umeme kwa Gesi Asilia  megawati 20 unaojulikana kitaalamu kwa jina la TM 2500 kutoka kituo cha Ubungo III jijini Dar es Salaam kwenda Mtwara.

Akizungumza Septemba 11, 2025 wakati wa zoezi la usafirishaji, Mhandisi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme Mtwara II, Godfrey Matiko, alisema mtambo huo una uwezo wa kuzalisha Megawati 20, na utaunganishwa na mtambo mwingine uliopo ambao tayari unazalisha Megawati 20 na hivyo kuongeza jumla ya uzalishaji kufikia Megawati 40 kwenye Kituo cha Uzalishaji Umeme kwa Gesi Asilia kilichopo eneo la Hiyari mkoani humo. 

Amesema, Umeme huo utasambazwa Mikoa ya Lindi na Mtwara ili kukidhi mahitaji ya matumizi ya umeme yanayoongezeka.

“Usafirishwaji wa mtambo huu unalenga kuongeza nguvu katika kituo cha Mtwara II, hivyo kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi na wawekezaji,” alieleza Mhandisi Matiko.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi kujipanga kunufaika na fursa za uwekezaji zitakazochochewa na upatikanaji wa umeme wa kutosha na wa uhakika.

Itakumbukwa kuwa mpaka sasa Mkoa wa Mtwara unauwezo wa kuzalisha umeme jumla ya megawati 50 kwa gesi asilia na uwepo wa mtambo huu mpya wa megawati 20 kutafanya uwezo wa uzalishaji umeme mkoani humo kufikia megawati 70.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...