Skip to main content

“NCHI YENYE MADINI YA KIPEKEE, KUWA NA WANANCHI MASIKINI NI AIBU” DOYO

 


Mwanza, Geita Buseresere 

Mgombea urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, akiendelea na kampeni zake Kanda ya Ziwa, amefanya mikutano ya hadhara katika Jimbo la Sengerema, eneo la Stendi ya Zamani, na Kata ya Buseresere, Mkoa wa Geita.

Katika hotuba yake, Mhe. Doyo aliwataka wananchi wa Kanda ya Ziwa kutafakari kwa kina juu ya sababu zinazowafanya kuendelea kukosa maendeleo licha ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kushika dola kwa zaidi ya miaka 60.

Mhe. Doyo aliwaahidi wananchi kuwa endapo watampa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atahakikisha wakulima wanapata fursa ya kuuza mazao yao katika masoko yenye tija na faida, badala ya kulazimishwa kuuza katika masoko yanayowanyonya na kuendeleza umaskini. 

“Wananchi, mkiniamini na kunipa kura Oktoba 29, nitasimamia na kuhakikisha wakulima wanapata bei nzuri na zenye motisha kwenye mazao yenu yote. Haiwezekani mtumie gharama kubwa katika kilimo chenu halafu mpangiwe bei, hizi ni mbinu za kuendeleza umaskini wenu ili CCM waendelee kuwatawala nyinyi na vizazi vyenu,” alisema Mhe. Doyo.

Aidha, Mhe. Doyo alizungumzia changamoto za miundombinu na huduma za kijamii wilayani Sengerema, akibainisha kuwa licha ya taifa kuwa na rasilimali nyingi kama dhahabu, almasi na tanzanite, bado wananchi wanaendelea kuishi maisha ya umaskini.

 “Nchi hii ina madini ya kila aina, lakini bado wananchi wake hawana maji safi, huduma bora za afya na miundombinu ya barabara. Hili ni jambo la aibu kubwa,” alisisitiza Doyo.

Akizungumzia sekta ya usafirishaji, Mhe. Doyo alisema madereva na wamiliki wa vyombo vya usafirishaji wamekuwa wakilalamikia gharama kubwa za uendeshaji kutokana na ubovu wa barabara, hali inayosababisha biashara zao kushindwa kuleta faida. Alisisitiza kuwa ni jambo lisilo sahihi kwa serikali kudai kodi kubwa kutoka kwa wafanyabiashara hao bila kuhakikisha uwekezaji kwenye barabara unafanyika ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato.

Mhe. Doyo aliendelea kusisitiza kuwa CCM imeshindwa kutatua changamoto hizi kwa miongo kadhaa, na sasa wanarudi tena kwa wananchi kuomba kura kwa hoja zilezile ambazo hawajawahi kuzitekeleza. Aliibua masuala ambayo yamekuwa kero kwa wananchi wa Sengerema na Buseresere Mkoa wa Geita, ikiwemo, Ubovu wa barabara, gharama kubwa za usafiri, Ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya afya, Upungufu wa maji safi na salama, Wakulima kushindwa kupata masoko yenye tija kwa mazao yao.

Kampeni za Mhe. Doyo zinaendelea, huku msafara wake ukielekea mkoani Kagera, Wilaya ya Ngara, kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...