Skip to main content

DOYO AAHIDI KUFUNGUA KIWANDA CHA KOROSHO TUNDURU NDANI YA SIKU 10


Ruvuma, Tunduru 

Msafara wa mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, umewasili katika wilaya ya Tunduru, mkoa wa Ruvuma, ambapo umefanya mkutano mkubwa wa kampeni.

Akihutubia wananchi wa Tunduru mjini katika viwanja vya Amazon na wananchi wa kijiji cha Nyakapanya, Mhe. Doyo aliwaahidi wananchi hao kuwa endapo watampa dhamana na ridhaa ya kuwa urais, atahakikisha anarejesha kiwanda cha kubagua korosho cha Wilaya ya Tunduru. Amesema kuwa kiwanda hicho kitakuwa nguzo muhimu ya kuinua uchumi wa wananchi wa Tunduru na kuchochea maendeleo ya mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Mhe. Doyo amesema kuwa utekelezaji wa mpango huo wa kufufua kiwanda ambacho thamani yake haizidi shilingi bilioni mbili, umekuwa ukikwamishwa na uzembe na dharau za viongozi wa chama tawala (CCM) kwa wananchi wa Tunduru. “Kama ukiangalia idadi ya mabango ya CCM, na kila bango moja lina thamani ya takribani shilingi elfu ishirini, utagundua kuwa tatizo si ukosefu wa fedha bali ni uzoefu wa kufanya mambo kwa mazoea. Miaka 60 ya utawala wao imekuwa ya kurudia makosa yale yale,” alisema Mhe. Doyo.

Aidha, Mhe. Doyo amewaahidi wananchi kuwa endapo watamchagua, kufufuliwa kwa kiwanda hicho kutachukua si zaidi ya siku 10, kwani tayari wapo wawekezaji walioonesha nia ya dhati ya kuwekeza. Ameongeza kuwa changamoto zilizokwamisha uwekezaji huo ni matokeo ya urasimu, ambao katika utawala wake utakomeshwa mara moja.

“Kiwanda hiki kitakuwa chanzo kikuu cha uchumi wetu. Haiwezekani fikra za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, za kuanzisha viwanda vya kuchakata korosho zipotee hivi hivi. Nichagueni, muone mabadiliko ya kweli,” alisisitiza Mhe. Doyo.

Akiendelea, Mhe. Doyo aliahidi kuwa serikali yake itawakopesha wananchi mashine ndogo za kubangua korosho ili kuongeza thamani ya mazao yao. Amesema hatua hiyo itasaidia wakulima kuuza korosho kwa hadi shilingi elfu ishirini (20,000) kwa kilo badala ya shilingi elfu mbili (2,000) wanazopata sasa. Amewaomba wananchi wa Tunduru na Ruvuma kwa ujumla kumfanyia kampeni za nyumba kwa nyumba, ili mabadiliko ya kiuchumi yaanze katika maisha ya mtu mmoja mmoja.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kigoda cha Kina Mama Taifa, Bi. Zaidat Fundi Majiamoto, amewataka kina mama wa Tunduru kujitokeza kwa wingi kumpigia kura Mhe. Doyo na Chama cha NLD, kwa kuwa chama hicho kinajali maslahi ya wananchi. Amesema changamoto kama kutembea umbali mrefu kutafuta maji, au kukosa vifaa vya uzazi hospitalini, ni ishara ya kudhalilisha utu wa mwanamke na si taswira nzuri katika jamii yetu. “Tumpigie kura Mhe. Doyo ili aondoe fedheha hizi na kuleta heshima kwa wanawake wa Tanzania,” alisema Bi. Majiamoto.

Naye Mhamasishaji Mkuu wa kampeni, Bi. Adija Dikulumbale, amesema kuwa wazee wa Ruvuma waliowahi kupigania uhuru wamesahauliwa, kwani maendeleo katika mkoa huo yamekwama kwa muda mrefu. “Huu ni muda wa mabadiliko. Mchagueni Doyo Hassan Doyo muone tofauti. Ameahidi kuleta mwekezaji ndani ya siku 10 na kuondoa urasimu unaokwamisha juhudi za kurejesha viwanda. Hii itazalisha ajira nyingi na kuongeza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja,” alisema Bi. Dikulumbale.

Msafara wa kampeni za Mhe. Doyo Hassan Doyo kupitia Chama cha NLD unaelekea katika wilaya Kirwa, Rufiji, Kibiti, Dar es Salaam na Morogoro.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...