Skip to main content

DOYO: AMANI NI NGUZO KUU YA MAENDELEO NA MAPINDUZI YA UCHUMI TANZANIA

 


Dar es Salaam 

Mgombea urais kupitia Chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, na Katibu Mkuu wa chama hicho, amewataka Watanzania kudumisha amani kabla, na baada ya uchaguzi mkuu ujao, akisisitiza kuwa amani ndiyo nguzo kuu ya maendeleo ya taifa lolote duniani.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa kampeni za chama hicho zinazofanyika kwa mtindo wa “mobile kampeni”, Doyo alisema chama chake kimefanya kampeni za kistaarabu na kisayansi katika mikoa 26 mpaka sasa. Alisema kampeni hizo zimekuwa zikiwalenga wananchi moja kwa moja ili kuwapa sera na kuelewa changamoto zao bila kutweza utu wa mtu.

“Niwaombe sana, Watanzania wenzangu, mkapige kura kwa amani. Mkivunja amani, hakuna maendeleo yatakayopatikana. Amani ndiyo tunu ya taifa letu,” alisema Mhe. Doyo.

Doyo alifafanua kuwa amani ni sharti muhimu la maendeleo. Alisema pale ambapo amani ipo, ndipo serikali inaweza kutekeleza kwa ufanisi ahadi zake kwa wananchi, ikiwemo kuboresha huduma za jamii, kukuza uchumi na kuongeza ajira.

Amani huleta utulivu wa kisiasa, hujenga imani kwa wawekezaji, na huipa serikali uwezo wa kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo bila vikwazo. Doyo alisema serikali isiyo na amani haiwezi kusimamia elimu bora, huduma za afya, wala uchumi imara.

“Amani huleta matumaini na nguvu ya kufanya kazi. Serikali itakayojengwa juu ya misingi ya amani itakuwa na uwezo wa kuwatumikia wananchi kwa haki na ufanisi mkubwa,” aliongeza Doyo.

Mhe. Doyo alisisitiza kuwa serikali atakayoiongoza itakuwa ya kuwakomboa Watanzania kiuchumi na kijamii, kwa kuweka mazingira bora ya vijana kujiajiri, kujitegemea na kuchochea ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja.

“Tunataka kuona kijana ana ajiriwa, anajiajiri na kuacha utegemezi. Serikali itakayojengwa juu ya amani itakuwa na nguvu ya kweli ya kuleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii,” alisema Doyo.

Akizungumza kuhusu Ilani ya Uchaguzi ya NLD, Doyo alisema chama chake kimeweka mkazo katika kumwezesha kijana wa Kitanzania kujitegemea, kukuza ujasiriamali na kujenga mazingira ya ajira. Alibainisha pia kuwa serikali yao itaweka kipaumbele katika kuboresha huduma za jamii kama elimu, afya na miundombinu, huku ikipunguza matumizi yasiyo ya lazima serikalini ili fedha hizo zielekezwe kwenye sekta zenye manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi.

“Hospitali hazina dawa, barabara hazijakamilika tangu uhuru. Tunataka serikali inayoweka kipaumbele katika maendeleo ya watu, si anasa,” alisisitiza Doyo.

Katika mkutano huo, Doyo alimnadi mgombea ubunge wa NLD Jimbo la Ubungo, Bi. Gradiness Msuya, akisema jimbo hilo limebaki nyuma kimaendeleo kutokana na miundombinu mibovu, shule zisizo na madawati na barabara zisizopitika. Aliwaomba wananchi wa jimbo hilo wamchague mbunge anayetokana na Chama cha NLD.

Kwa upande wake, Bi. Msuya aliwataka wananchi wa Ubungo kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa amani na busara, ili kuleta mabadiliko ya kweli na maendeleo ya jimbo hilo.

“Niwaombe tarehe 29 Oktoba msifanye makosa. Tukiungana tutaleta mageuzi katika nchi yetu, lakini pia tuijenge Ubungo yetu,” alisema Bi. Msuya.

Bi. Msuya aliwaomba kura wananchi wa Jimbo la Ubungo, huku akiwahidi kushirikiana nao kusukuma maendeleo ya jimbo hilo kwa vitendo.

Naye Meneja kampeni wa Chama cha NLD, Ndugu Pogora Ibrahim Pogola, alieleza kuwa chama hicho kimetumia mbinu mpya za “mobile kampeni” katika uchaguzi huu, mbinu iliyolenga kuwafikia wananchi, badala ya kutumia mikutano mikubwa yenye gharama kubwa, ikizingatiwa kuwa wananchi wengi wanaishi maisha ya kipato cha chini. 

“Tunafanya kampeni za kisayansi. Hatuleti wasanii wala kubeba wananchi kwa magari. Tunawafuata wananchi walipo ili tusikilize matatizo yao na kuwaeleza sera zinazotokana na ilani yetu moja kwa moja,” alisema Pogola.

Ameongeza kuwa Ilani ya NLD inalenga kupunguza maslahi makubwa ya wabunge na kuelekeza fedha hizo katika kuongeza mishahara ya walimu, madaktari na watumishi wa umma.

“Chama chetu kimekuja na ilani bora, inayolenga maendeleo ya watu. Tukipiga kura kwa amani, mkituchagua NLD, sera za chama chetu zote zinatekelezeka kwa ufanisi,” alihitimisha Pogola.

Msafara wa kampeni za chama cha NLD unaelekea Mtwara na Zanzibar katika muendelezo wa kuwataka wananchi kuchagua viongozi waadilifu wanaotokana na chama cha NLD katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...