Skip to main content

WAMAMA 137 WANUFAIKA NA ELIMU YA POLIO HOSPITALI YA RUFAA MWANYAMALA

 



Na Mwandishi. Wetu --Dar es salaam

Ikiwa zimesalia siku kadhaa Tanzania kuungana na nchi zingine duniani kuadhimisha siku ya Polio duniani Oktoba 24, 2025, klabu ya Rotary Mikocheni imetoa hamasa kwa wakina mama 137 kuhakikisha wanapojifungua watoto wao wanapata chanjo zote ikiwemo ya Polio wanapofikisha miezi 6 ili wawe salama.

Ameyasema hayo Oktoba 2025, Rais wa Klabu ya Rotary Mikocheni Nasibu Mahinya katika Hospitali ya Rufaa Mwananyamala jijini Dar es salaam wakati wakihamasisha wakina mama kuhudhuria kliniki mara baada ya kujifungua ili watoto wao wapatiwe chanjo zote kuwaepusha na magonjwa yanayoweza epukika ikiwemo polio.

"Hii ni wiki ya nane ya kampeni ya ‘Mama, Mkinge Mwanao!’ ambayo klabu ya Rotary tumeanzisha kwa kujitolea kuhamasisha wakina mama juu ya umuhimu wa chanjo ya Polio kwa wamama waliojifungua ili wahakikishe mara baada ya kuzaliwa watoto wao wanapata chanjo zote nne za Polio." Amesema rais Nasibu

Sambamba na hayo amebainisha kuwa Polio ni ugonjwa hatari unaosababisha kupooza na kusabisha mtoto kushindwa kutembea hivyo amewasisitiza wakina mama kuhakikisha wanafika vituo vya afya kupata chanjo kwani ni buree kabisa bila malipo.

Kwa Upande wake mhamasishaji wa kujitolea na mwanafunzi kutoka Chuo cha Kampala cha Tanzania Kennedy Munisi amesema kundi la watoto wachanga wanaozaliwa wako hatarini kupata ugonjwa wa polio, hivyo ndiyo maana Serikali inatoa chanjo bure za matone kwa watoto wachanga.

Pia ugonjwa huo unaambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na unashambulia mfumo wa hewa na chakula hivyo chafya kukohoa majimaji yakimpata mtu ambaye hujawahi kupata chanjo unaweza kumletea maambukizi.

Kampeni hii ya Mama, Mkinge Mwanao, inaendeshwa kwa ushirikiano wa klabu ya Rotary Mikocheni na klabu za Rotaract za Tanzania ikiwemo Rotaract klabu ya Kampala (KIUT).

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...