DIWANI JESCA MAHMOUD MSOLLA AZINDUA KLINIKI YA VYETI VYA KUZALIWA BUYUNI
Na AyraNewstz
DIWANI wa kata ya Buyuni Wilayani Ilala Mkoa Dar es Salaam, JESCA MAHMOUD MSOLLA, amezindua Kiliniki ya vyeti vya kuzaliwa kata ya Buyuni kwa ajili ya kuwasogezea wananchi huduma za kijamii karibu na makazi yao.
Kampeni hiyo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa ambayo itakuwa wa siku kumi kutoa huduma ofisi za Afisa Mtendaji wa kata ya Buyuni ilianza Mei 13 itaendelea mpaka Mei 24 mwaka huu .
Akizungumza kwa niaba ya Diwani wa Buyuni, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Buyuni ,Sylvanus Benard Mwenda ,alisema zoezi hilo limeratibiwa na Diwani Jesca Mohmoud Msola kwa ajili ya kutatua kero za wananchi wake sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM .
"Diwani Jesca Mohmoud Msola, ameiona hii changamoto kubwa ya vyeti vya kuzaliwa ndio akabeba jukumu la kuleta RITA waweze kutoa vyeti vyeti vya kuzaliwa vinatolewa hapo hapo kwa gharama za Serikali "amesema Mwenda.
Mwenda amesema katika Jamii lazima uwe na vyeti vya kuzaliwa ili uweze kupata huduma nyingine ikiwemo kuomba Kitamburisho cha Taifa NIDA au hati ya kusafiria..
Aidha amesema zipo changamoto zingine shule na vyuoni wanafunzi wengi hawana vyeti hivyo kulazimika kupata usumbufu wa baadhi ya huduma.
Alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na RITA kwa kusogeza huduma hiyo ya vyeti vya kuzaliwa .
Kwa upande wake Mratibu wa Kampeni ya Kliniki ya Rita Wilayani Ilala Heri shaban amesema dhumuni la kupeleka huduma hiyo kusajiliwa wananchi vyeti vya kuzaliwa awali kulikuwa na Kliniki ya Vitamburisho vya TAIFA NIDA akakumbana na changamoto kubwa wananchi wengi vyeti vya kuzaliwa walikuwa hawana hivyo ikapelekea kukosa fursa ya kupata NIDA ikalazimika kuomba maombi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kuomba RITA wafike Kata za pembezoni kutoa hiduma .
Kwa upande wake Afisa Msajili wa Vyeti vya kuzaliwa Rita ,Erasto wambura amesema dhumuni la kampeni hiyo kusaidia Serikali kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwa cheti cha kuzaliwa kinasaidia mambo mengi Kliniki ya Rita kwa sasa wameweka Kambi Buyuni,Chanika na Gongolamboto Ofisi za Serikali amewataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo.
Afisa Wambura amesema dhumuni la Kliniki ya Rita kuwafikia watu wengi zaidi ,aliwataka wananchi kubeba nyaraka zote za muhimu ikiwemo taarifa za Wazazi,Tangazo,kadi ya mimba na kadi ya Kliniki au cheti cha ubatizo.

Comments
Post a Comment