Skip to main content

LONDO - VIPIMO SAHIHI NI MSINGI WA UCHUMI WA VIWANDA NA TEKNOLOJIA

 


Na Habar Plus

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuimarisha mifumo ya vipimo nchini ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kimataifa, kukuza viwanda na kujenga uchumi wa kisasa unaotegemea sayansi na teknolojia.

Mhe. Londo ametoa kauli hiyo leo Mei 20,2026 jijini Dodoma wakati akifunga rasmi maadhimisho ya Siku ya Vipimo Duniani ambapo amesisitiza kuwa maendeleo ya viwanda, biashara na huduma bora hayawezi kufikiwa bila uwepo wa vipimo sahihi na vinavyoaminika.

Amesema serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kisera na kisheria ili kuwezesha biashara, kuvutia uwekezaji na kuongeza ufanisi wa sekta binafsi kwa kuzingatia matumizi ya vipimo vinavyokubalika kitaifa na kimataifa.

“Hakuna biashara yenye uaminifu bila vipimo sahihi, hakuna viwanda vinavyoweza kushindana kimataifa bila mifumo sahihi ya vipimo, na hakuna sera bora bila taarifa sahihi zinazotokana na sayansi ya vipimo,” amesema Mhe. Londo.

Hata hivyo amezitaka taasisi za serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kuendelea kushirikiana katika kuimarisha matumizi ya vipimo sahihi ili kuongeza uwazi, ufanisi na uaminifu katika maamuzi ya kitaifa.

Amesema maadhimisho ya mwaka huu yamebeba ujumbe muhimu unaolenga kuonesha namna sayansi ya vipimo inavyoweza kusaidia kujenga imani katika uandaaji wa sera na utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

Akizungumzia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,Mhe. Londo amesema Tanzania haiwezi kufikia uchumi wa viwanda na teknolojia bila kuwa na mifumo madhubuti ya vipimo, maabara za kisasa pamoja na wataalamu wenye ujuzi wa kimataifa.

Amesema vipimo vina mchango mkubwa katika kuongeza tija viwandani, kuchochea ubunifu, kulinda afya za wananchi na kuimarisha biashara ya kimataifa.

“Tunapozungumzia Tanzania ya viwanda, bidhaa zenye ushindani na huduma bora, tunapaswa kutambua kuwa msingi wake ni vipimo sahihi na vya kuaminika,” amesisitiza.

Aidha amesema serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza katika taasisi za udhibiti na mifumo ya kisasa ya vipimo ili kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa na huduma zenye ubora unaostahili..

Hata hivyo ameutaka Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) kuendelea kusimamia haki katika matumizi ya vipimo ili wananchi wapate bidhaa kulingana na thamani halisi ya fedha wanazolipia na kudhibiti udanganyifu katika biashara.

Pia ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuendelea kuimarisha maabara za kitaifa, mifumo ya ithibati na ulinganifu wa vipimo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Kwa upande wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), amesema kinapaswa kuongeza programu za mafunzo zinazohusiana na vipimo, tathmini ya ubora na uandaaji wa sera ili kuzalisha wataalamu watakaosaidia kuunganisha sayansi na maendeleo ya uchumi.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...