Skip to main content

TFS YATAKA VIWANGO VYA UBORA VILINDWE KATIKA BIASHARA YA ASALI

 




Tabora, Mei 21, 2026

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umewataka wananchi wanaojihusisha na ufugaji nyuki na uchakataji wa mazao yatokanayo na nyuki kuzingatia viwango vya ubora na usalama wa bidhaa zao, ukionya kuwa uzalishaji usiozingatia sheria unaweza kuhatarisha masoko ya ndani na nje ya nchi.

Tahadhari hiyo ilitolewa leo na Meneja wa Rasilimali Nyuki wa TFS, SACC Hussein Msuya, wakati wa majadiliano ya biashara kwa biashara na mdahalo kuhusu maendeleo ya sekta ya ufugaji nyuki nchini, uliofanyika katika Viwanja vya Kumbukumbu ya Vita mkoani Tabora kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani.

SACC Msuya alisema Tanzania imeendelea kujijengea sifa kimataifa kutokana na ubora wa mazao yake ya nyuki, hususan asali na nta, lakini akasisitiza kuwa ubora huo unaweza kupotea iwapo wafugaji na wachakataji hawatazingatia viwango vilivyowekwa na mamlaka husika.

“Utumiaji wa vifungashi bora ni takwa la kisheria na unasimamiwa na sheria ya viwango. Kwa mujibu wa kanuni za ufugaji nyuki, asali lazima ifungashwe kwa ubora na iwekwe lebo kwa mujibu wa Kanuni ya 21 ya ufugaji wa nyuki,” alisema SACC Msuya.

Alisema baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta hiyo ni pamoja na matumizi ya vifungashio visivyokidhi viwango, uchakataji usiozingatia usafi pamoja na uhifadhi usiofaa wa bidhaa za nyuki, hali inayoweza kushusha ubora wa bidhaa na kupunguza imani ya wanunuzi.

Aidha, aliwataka wananchi kutumia vifaa sahihi wakati wa uvunaji na uchakataji wa asali, nta na gundi ya nyuki ili kuhakikisha bidhaa hizo zinadumu katika ubora unaokubalika kwenye soko la ushindani.

“Wito wangu kwa wananchi ni kujikita katika matumizi ya vifungashio vilivyoidhinishwa na vinavyokidhi viwango vya ubora na usalama wa asali,” alisisitiza.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wa mdahalo huo waliishukuru TFS kwa kuendelea kutoa elimu ya ufugaji bora wa nyuki, wakisema mafunzo hayo yatawawezesha kuongeza uzalishaji wa bidhaa zenye ubora na kuongeza kipato cha kaya zao.

Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani yanaendelea katika Viwanja vya Kumbukumbu ya Vita mkoani Tabora, huku wananchi wakihamasishwa kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ili kujifunza teknolojia za kisasa za ufugaji nyuki na kushiriki kilele cha maadhimisho hayo kitakachofanyika kesho Mei 22, 2026.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...