Skip to main content

ILI KUFIKIA UMEME WA MEGAWATI 8,000 IFIKAPO 2030; NDEJEMBI ATAJA VYANZO




Waziri wa Nishati, Mhe.Deogratius Ndejembi, amesema Serikali imejipanga kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawati 4,300 za sasa hadi kufikia megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030 kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali mikubwa ya uzalishaji wa umeme nchini.

Amesema hayo akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 Bungeni jijini Dodoma

Akifafanua kuhusu hilo amesema kuwa, Dira ya Taifa imeweka lengo la kufikia uzalishaji wa megawati 74,000 za umeme ifikapo mwaka 2050, huku maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yakielekeza Taifa kufikia angalau megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030.

Mhe.Ndejembi amesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara ya Nishati imeweka mikakati madhubuti ya kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme itakayosaidia kufikia lengo hilo.

Miongoni mwa miradi hiyo ni mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia nishati ya jua wa megawati 100 katika eneo la Kishapu mkoani Shinyanga, ambao aliutaja kuwa wa kihistoria kutokana na ukubwa wake.

Amssema tayari megawati 50 zimeanza kupatikana kupitia mradi huo na kwamba uzalishaji wa megawati zote 100 unatarajiwa kuanza ndani ya mwaka wa fedha 2026/2027.

Ndejembi pia ametangaza kuanza kwa utekelezaji wa mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa megawati 2,000 kwa kutumia makaa ya mawe katika eneo la Mchuchuma wilayani Ludewa mkoani Njombe.

Amesema licha ya Tanzania kuwa na hifadhi kubwa ya makaa ya mawe, bado nchi haijaanza kuzalisha umeme kupitia rasilimali hiyo, jambo ambalo Serikali sasa inalikwenda kulibadilisha kupitia mradi huo mkubwa.

“Taifa letu lina hifadhi kubwa ya makaa ya mawe lakini hatuzalishi hata megawati moja kwa kutumia makaa ya mawe. Sasa tunaanza utekelezaji wa mradi huu wa megawati 2,000 katika eneo la Mchuchuma,” amesema

Aidha, amesema Serikali itaendelea kuongeza vyanzo vya uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia kwa kutekeleza mradi wa Kinyerezi III ambao unatarajiwa kuzalisha megawati 1,000 na kuziingiza katika Gridi ya Taifa.

Miradi mingine inayotarajiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027 ni pamoja na Mradi wa Umeme wa Kakono wenye uwezo wa kuzalisha megawati 87 pamoja na Mradi wa Malagarasi ambao unaendelea na utekelezaji wake.

Kwa mujibu wa Waziri Ndejembi, utekelezaji wa miradi hiyo utaongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini, kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na kusaidia Tanzania kufikia malengo ya maendeleo yaliyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...