Skip to main content

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE




Na Mwandishi wetu,

Rufiji - Pwani

Madiwani wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani Katavi, wakiongozana na baadhi ya wabunge na viongozi wengine, wamepongeza uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) baada ya kujionea kwa karibu uendeshaji wa kituo hicho na mchango wake katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini.

Viongozi hao walitembelea kituo hicho tarehe 20 Juni 2026 kwa lengo la kujionea uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, kufahamu namna kituo kinavyoendeshwa pamoja na kupata uelewa wa mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini. Ziara hiyo ilihusisha madiwani 22 pamoja na baadhi ya wabunge na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Katavi.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda, Charles Philipo, aliishukuru Serikali kwa juhudi kubwa inazoendelea kufanya katika kuimarisha sekta ya nishati na kuipongeza TANESCO kwa kuwapatia viongozi hao fursa ya kujionea kituo hicho.

“Tunaishukuru Serikali yetu kwa namna ambavyo imejikita kutatua changamoto ya umeme. Nipende kuwashukuru TANESCO kwa niaba ya waheshimiwa madiwani wa Mpanda na Nsimbo kwa kuona namna ya sisi kuja hapa na kujionea kituo hiki,” alisema Philipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, Mhe. Anna Mpembe, alisema ameoneshwa kuvutiwa na ukubwa wa kituo hicho na kiwango cha uwekezaji kilichowekwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa kutosha kwa maendeleo ya taifa.

“Leo tunaona maajabu na miujiza kupitia Kituo cha Julius Nyerere. Jinsi kilivyojengwa ni kitu cha thamani kubwa sana katika nchi yetu ya Tanzania,” alisema Mhe. Mpembe.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda, Joseph Lwamba, alisema maendeleo ya sekta ya umeme yameendelea kubadilisha maisha ya wananchi kwa kuongeza fursa za kiuchumi na kijamii katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi.

“Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba katika wilaya yetu ya Mpanda karibu vijiji vyote sasa vina umeme. Wananchi wanaweza kufanya shughuli zao za maendeleo kupitia umeme huu,” alisema Lwamba.

Akielezea lengo la ziara hiyo, Mhandisi wa Usafirishaji Umeme Mkoa wa Katavi, Victor Ngw'igulu, alisema viongozi hao wameletwa katika kituo hicho ili kujionea kwa macho maendeleo makubwa yanayofanywa na Serikali kupitia sekta ya nishati na kuwa mabalozi wa kueleza wananchi mafanikio hayo.

“Wananchi wanapaswa kujua nini kinafanywa na TANESCO kupitia Wizara ya Nishati na hii ni sehemu nzuri ya kuona maendeleo yanayofanywa katika nchi yao. Kupitia Mkoa wa Katavi tumewaleta waheshimiwa hawa ili wajionee kwa macho kile walichokuwa wanakisikia kuhusu Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere, namna kinavyofanya kazi na kuchangia katika uchumi wa taifa,” alisema Ngw'igulu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere, Mhandisi Elinainyi Kalalu, alisema ujio wa viongozi hao una mchango mkubwa katika kuendelea kuhamasisha uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kituo hicho na nafasi yake katika maendeleo ya taifa.

“Tumewapitisha katika maeneo mbalimbali na kuwaonyesha miundombinu inayotumika katika uzalishaji wa umeme. Tuna imani kwamba wataichukulia ziara hii kama chachu ya maendeleo na watakuwa wajumbe wazuri huko waendako, hasa katika kuelezea mchango wa Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere katika maendeleo ya taifa,” alisema Kalalu.

Ziara hiyo imewapa madiwani wa Mpanda na Nsimbo pamoja na viongozi wengine kutoka Mkoa wa Katavi fursa ya kujionea kwa karibu uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya nishati kupitia Kituo cha Kufua Umeme cha Julius Nyerere. Aidha, viongozi hao wameeleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa na kuahidi kuendelea kuhamasisha wananchi kutambua mchango wa kituo hicho katika kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

Comments

Popular posts from this blog

MWAKIPOSA MWENYEKITI MPYA WA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA DAR

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Boko Wilaya ya Kinondoni, Razalous Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam kwa kupata kura 24 kati ya 37 zilizopigwa na wajumbe mapema leo hii. Uchaguzi huo umemalizika leo June 20, 2026ambapo  ulikua unahusisha nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu, ambapo Mwenyekiti ameshinda Razalous Mwakiposa huku Katibu Mkuu akiwa ni Peppino Sudi Peppino . Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi, Kambi Sinde, amesema kuwa Razalous Mwakiposa ameshinda kwa kupata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akishinda kwa kura 20 kati ya kura 37 zilizopigwa. "Uchaguzi umefanyika kwa uwazi na haki, kulikuwa na jumla ya wajumbe 40, lakini watatu walipata udhuru, hivyo, leo waliopiga kura ni wajumbe 37 na matokeo ni kwamba mshindi wa nafasi ya Mwenyekiti amepata kura 24 kati ya kura 37 zilizopigwa, huku Katibu Mkuu akipata kura 20 kati ya kura 37 zilizop...

TIRDO YAVUNJA VIKWAZO VYA UBUNIFU, AFRO HEAL YAGEUZA MIMEA YA ASILI KUWA DAWA ZA KISASA

Na Ayra News.  Mashauri Enock Shushu, kutoka Afro heal Group Limited, amesema malezi ya ubunifu kupitia shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) yameiwezeshaa kampuni hiyo kubadili dawa za asili zilizokuwa zikitengenezwa kwa kutumia magome ya miti na kuzigeuza kuwa bidhaa za kisasa zinazokidhi viwango vya ubora na mahitaji utengenezaji soko. Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane 2026, Shushu alisema Afro healGroup Limited ni kampuni inayojihusisha na utafiti na utengenezaji wa dawa za binadamu zinazotokana na mimea ya asili, huku TIRDO ikiwa imekuwa nguzo muhimu katika kukuza uwezo wao wa ubunifu na uzalishaji. Alisema kabla ya kujiunga na TIRDO, kampuni hiyo ilikuwa ikitengeneza dawa za asili katika mfumo wa magome, lakini baada ya kupata malezi ya biashara, ushauri wa kitaalamu na uwekezaji wa rasilimali watu kupitia taasisi hiyo, imefanikiwa kuziboresha na kuzalisha bidhaa za kisasa zinazorahisisha matumizi kwa wananchi. Shushu alisema ushirikiano kati ya wa...

VETA KAGERA WABUNI MTEGO KISASA WA KUVUNA SENENE

Ayra Nwestz  Chuo cha Veta mkoa wa Kagera VTC kimebuni mtambo wa kisasa wa kuvuna senene ambao unamuwezesha mvunaji kunapata senene wengi kwa wakati mmoja ambao wanakua salama. Akizungumza na Mtandao wa Matukio Daima, katika maonyesho ya 47 ya biashara ya kimataifa, Mwalimu wa Kagera VTC, Elias Lucas Mayala, amesema chuo hicho kimebuni mtego huo una lengo la kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na mbinu za jadi za uvunaji. Mayala amesema kuwa mtanbo huo una uwezo wa kubeba kati ya kilo 80 hadi 100 za senene kwa wakati mmoja wakati wa uvunaji.  Aidha, amesema mtego huo una mfumo wa kuchuja senene wanapoingia na kuwatenganisha wadudu wadogo wadogo, ambao wanaweza kutumika kama chakula cha kuku badala ya kutupwa. Ameeleza kuwa tofauti na mbinu za zamani zinazoweza kuharibu miti na mazalia ya senene, mtego huo ni rafiki wa mazingira na umeundwa kwa namna inayorahisisha matumizi yake, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kusogezwa kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na mahitaji...